Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Wednesday, August 21, 2013

MAANDALIZI YA MICHUANO YA CHANETA TAIFA ITAKAYOFANYIKA JIJINI MBEYA

MAFUNDI WAKIENDELEA NA UKARABATI WA KIWANJA CHA PILI KWAAJILI YA MICHUANO YA CHANETA ITAKAYOANZA KUTIMUA VUMBI SIKU YA JUMAMOSI LAKINI UZINDUZI RASMI NI JUMAPILI YA WIKI HII NDANI YA UWANJA WA SOKOINE JIJINI MBEYA.UWANJA MMOJA TAYARI UMEKAMILIKA KAMA UNAVYOONEKANA HAPA CHINIZIKIWA zimesalia siku chache kuanza kwa mashindano ya mchezo wa Netiboli taifa,maandalizi ya mashindano hayo yametajwa kuwa ya kususua kwa kiasi kikubwa. Mwenyekiti wa Chama cha Netiboli(Chaneta) mkoani Mbeya Mary Mng’ong’o alithibitisha kusuasua kwa maandalizi hayo alipozungumza na Lyamba Lya Mfipa. Mng’ong’o amesema sababu ya kusuasua huko ni kukosekana kwa fedha kwaajili ya maandalizi hali aliyosema inatokana na wadau waliokuwa wakitegemewa kuchangia kutotimiza ahadi zao kwa wakati. Kwa mujibu wa mwenyekiti huyo hadi jana zilikiwa kimekusanywa kiasi cha fedha kisichofikia hata laki tano ilikhali kiasi cha fedha kinachohitajika ni zaidi ya shilingi milioni 16. Amesema wapo pia baadhi ya wadau ambao ni wajumbe wa kamati ya maandalizi walioahidi kuchangia kiasi cha fedha kwaajili ya kusaidia kufanikisha mashindabno lakini wao pia hawajachangia na kila wanapopigiwa simu wamekuwa wakieleza kutingwa na mambo yao binafsi. Aliwaomba wadau mbalimbali walioahidi kusaidia,kutimiza ahadi zao huku pia akisema serikali inapaswa kuliona suala la uandaaji mashindano kama hayo kwa namna nyingine itakayowapungumzia ugumu waandaaji wanaoelemewa na mzigo huo. Lyamba Lya Mfipa pia imefika katika viwanja vya mchezo huo vilivyopo ndani ya uwanja wa Sokoine jijini Mbeya na kuwakuta mafundi wakiendelea na ukarabati wa viwanja hivyo.

No comments:

Post a Comment