Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, August 9, 2013

PSPF YAKUTANA NA WADAU MKOANI MBEYA

WADAU wa mfuko wa pensheni kwa watumishi wa umma(PSPF) mkoani Mbeya wameupongeza mfuko huo kwa kuanzisha mpango wa kukutana na wadau mbalimbali na kuwaongezea uelewa juu ya mifuko ya jamii. Wadau hao walitoa maoni yao kwenye warsha fupi iliyofanyika katika hoteli ya Hill View iliyopo jijini Mbeya ikiwakutanisha viongozi wa PSPF na wadau. Wadau hao walisema mfumo wa kukutana na wadau ni jambo muhimu kwakuwa itasaidia kupunguza malalamiko yanayotokana na uelewa mdogo walionao watumishi juu ya mifuko ya hifadhi za kijamii. Mmoja wa wadau hao afisa utumishi wa halmashauri ya wilaya ya Mbeya Kateti Seleman,alisema mpango wa PSPF wa kukutana na wawakilishi wa watumishi unapaswa kuigwa na viongozi wa mifuko mingine. “Tumekuwa tukishuhudia kwa muda mrefu wenzenu wakikutana na wakurugenzi pekee.Wao wanaamini kwa kukutana na hao wanakuwa wamekamilisha mambo.Lakini si kweli.Wazo mlilokuja nalo hili la kukutana na watumishi na waajiri ni la msingi zaidi” alisema. Akizungumzia lengo la warsha hiyo mjumbe wa bodi ya PSPF Clement Mswanyana alisema mifuko ya hifadhi za jamiibado haijaeleweka kwa wananchi wengi nchini. “Wapo watumishi ambao wanakosa mafao yao kwa kukosa taarifa sahihi za mifuko.Ndiyo sababu tumeamua kuanzisha utaratibu huu wa kukutana na wadau ili kuongezeana uelewa.Wapo watumishi pia ambao wanapoingia kwenye ajira wamekuwa wakipewa taarifa potofu” alisema Mswanyana. Mswanyana pia alilalamikia uwepo wa waajiri hususani maafisa utumishi ambao wamekuwa wakiomba rushwa kutoka kwa maafisa mbalimbali wa mifuko ili waweze kuwaruhusu watumishi wao kujiunga na mifuko husika. Naye afisa msimamizi wa PSPF mkoani hapa Niteko Chaula alizungumzia fao la elimu,la ujasiriamali na fao la kujitoa kuwa huduma mpya ambazo zimeanzishwa na mfuko kwaajili ya kuboresha zaidi maisha ya watumishi. Akizungumzia mkopo wa nyumba,Chaula alisema mfuko huko baada ya kujenga katika mikoa mingi nchini unataraji kujenga mkoani Mbeya lakini akasisitiza kuwa ujenzi wa ofisi ni jambo litakalotangulia ili kuondokana na gharama za pango.

No comments:

Post a Comment