Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, August 2, 2013

MADIWANI NA WAKUU WA IDARA HALMASHAURI YA JIJI LA MBEYA WATIMULIWA KWENYE KIKAO CHA KAMATI YA LAAC

KAMATI ya bunge ya hesabu za (LAAC) jana ililazimika kuwatimua kwa muda madiwani na wakuu wa idaya za halmashauri ya jiji la Mbeya kwenye kikao cha kupitia taarifa za matumizi ya fedha za umma kwenye utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo. Kamati ililazimika kuwaondoa kwenye kikao watu hao kufuatia kuwepo kwa mkanganyiko wa maelezo kwenye vitabu vya taarifa za matumizi hayo ambapo vitabu vya wajumbe wa kamati vilikuwa na maelezo sawa na vile vya maofisa kutoka ofisi ya mkaguzi wa hesabu za serikali(CAG) lakini vikatofautiana na vitabu walivyokuwa nanvyo wakuu wa idara. Hoja ya matumizi ya kiasi cha shilingi milioni 104 kwaajili ya ukarabati wa mabweni ya Kawawa na Sokoine kwenye shule ya sekondari ya Iyunga iliyopo jijini hapa ndiyo iliyozua mgogoro na kukatisha kikao kwa muda. Taarifa za CAG zilionesha zilionesha kuwa hadi ukaguzi unafanyika bweni moja lilikuwa limekarabatiwa lakini fedha zote zilionekana kutotumika bado huku pia kukiwa hakuna mkataba uliowekwa kati ya halmashauri na mkandarasi aliyepewa kazi hiyo na muda wa mkataba haukujulikana. Katika harakati za kuijibu hoja hizo ndipo wakuu wa idara akiwemo mweka hazina James Jorojike na madiwani wakiongozwa na meya Athanas Kapunga walipoanza kujichanganya kwa kutoa majibu yanayokinzana hali iliyosababi mwenyekiti wa Laac Rajab Mohamed kuahirisha kwa muda kikao na kuomba madiwani na wakuu wa idara watoke nje ya ukumbu kuanzia saa 7:40 hadi saa 8:9 mchana. “Tuna takriban hoja 25,bado tupo kwenye hoja moja ambayo tumeshindwa kukubaliana.Taarifa mliyompa ninyi wenyewe CAG inaonesha bweni moja limekarabatiwa lakini fedha zote zipo.Tunataka kujua fedha mlizotumia mlitoa wapi.Ninyi manasema mabweni yote yamekarabatiwa na fedha zimetumika.Naomba tubaki wabunge tujadiliane tuone nini kifanyike” alisema Mohamed kabla ya kuwatoa nje madiwani na wakuu wa idara. Hata hivyo baada ya kurejea ukumbini,mwenyekiti huyo alisema wabunge walikubaliana kutoa maagizo siku ya maazimisho ya ziara yote kwa mkoa wa Mbeya itakayofanyika Agosti 3 mwaka huu katika ofisi ya mkoa.

No comments:

Post a Comment