Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, July 30, 2013

MTOTO AUAWA KWA KUCHINJWA SHINGO BAADA YA KUBAKWA

MTOTO wa miaka sita amebakwa na kisha kuuawa kikatili kwa kukatwa shingo na mkono kwa panga na kijana mwenye umri wa miaka 14. Tukio hilo la kusikitisha limetokea Julai 29 mwaka huu majira ya saa 11 jioni katika kijiji cha Ijoka kata ya Mpombo wilayani Rungwe wilaya ambayo inashiriki katika kuendesha mradi wa majaribio wa kupinga ukatili wa jinsia na watoto(GBV) unaoendeshwa na shirika la Watereed kwa ufadhili wa watu wa marekani kupitia mfuko wa rais wan chi hiyo. Kamanda wa polisi mkoani Mbeya Diwan Athumani alimtaja mtoto aliyetendewa ukatili huo kuwa ni Janeth Mwailima mkazi wa Ijoka ambapo kabla ya kuawa alibakwa. Alimtaja mtuhumiwa wa vitendo hivyo vya kinyama kuwa Narbeth Haule anayedaiwa kuwa mkulima na mkazi wa kijiji cha Ijoka hali inayodhihirisha alitenda unyama huo pasipokujali udugu wa kuheshimiana na kusaidiana katika mambo mbalimbali ambao wamekuwa nao wakazi wa vijiji vya wilayani Rungwe na mkoa wa Mbeya kwa ujumla. Kamanda Athuman alisema awali baada ya kubakwa mtoto Janeth aliapa kwenda kuwaambia wazazi wake akiwemo baba yake juu ya unyama aliotendewa na ndipo kijana huyo aliamua kwenda nyumbani kwao kuchukua upanga na kuja kumkata mtoto huyo shingoni na mkono wake wa kulia lengo likiwa ni kupoteza ushahidi wa kubaka. Alisema tayari jeshi hilo linamshikilia kijana huyo na kuwa taratibi mbalimbali za kisheria zinaandaliwa ili aweze kufikishwa mahakamani na mkono wa sheria kuchukua mkondo wake kwa roho ya unkatili na unyama aliyo nayo dhidi ya binadamu wenzake. “Lengo lake ilikuwa kupoteza ushahidi kwakuwa mtoto aliyembaka alitishia kwenda kuwaeleza wazazi wake juu ya aliyotendewa na mkazi mwenzao.Lakini badala ya kupoteza ushahidi amezidi kujiweka matatani” alisema kamanda.

No comments:

Post a Comment