Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, July 5, 2013

MRADI WA KUPINGA UNYANYASAJI WA KIJINSIA(GBV) WAZINDULIWA TUKUYU RUNGWE

Wafanyakari wa shirika na Watereeda na wa kikundi cha huduma za majumbani(Kihumbe) Kushoto wakishindana kuvuta kamba na Watumishi wa serikali wa halmashauri ya wilaya ya Rungwe kwenye uzinduzi wa Mradi wa majaribio wa kupinga Ukatili wa kijinsia(GBV) unaofadhiliwa na mfuko wa rais wa arekani.Shindano lilimalizika kwa upande wa Watereed na Kihumbe kushindaMkuu wa chuo cha Magereza cha Kiwira Kamishina Msaidizi Mwandamizi Stanford Ntirundura akikabidhi kombe kwa nahodha wa timu ya soka ya Tukuyu Stars Afrika Ambele kombe baada ya timu hiyo kuifunga Mpuguso Stars goli 4-2 katika mchezo uliochezwa kwenye uzindizi wa mradi wa majaribio wa kupinga Ukatili wa kijinsia(GBV) unaofadhiliwa na mfuko wa rais wa arekaniNahodha wa timu ya netiboli ya Tukuyu Queens Rehema Mwambusi akionesha kombe kwa wachezaji wenzake(hawapo pichani) baada ya kukabidhiwa na Mkuu wa chuo cha Magereza cha Kiwira Kamishina Msaidizi Mwandamizi Stanford Ntirundura baada ya timu hiyo kuifunga goli 20-10 timu ya Magereza Queens kwenye uzindizi wa mradi wa majaribio wa kupinga Ukatili wa kijinsia(GBV) unaofadhiliwa na mfuko wa rais wa arekani.MMOJA WA WARATIBU WA GBV HIJJA WAZEE AKIUTAMBULISHA MRADI KWA WAKAZI WILAYANI RUNGWE KABLA YA MGENI RASMI KUUZINDUA WACHEZAJI WA TIMU ZA NETIBOLI WAKIFANYA MAZOEZI KABLA YA KUINGIA KATIKA MTANANGE WA KUMPATA BINGWA WA GBV KWA WANAWAKEBURUDANI YA IGIZO KUTOKA KWA WASANII WA KIKUNDI CHA KIHUMBE ILIKUWA KIVUTIO KINGINE KILICHOVUTA HISIA ZA WENGI WALIOHUDHURIA KUTAKASWA kwa mwanamke aliyefiwa na mumewe kumetajwa kuwa sehemu ya mila potofu zinazoendeleza unyanyasaji wa kijinsia kwa wanawake wilayani Rungwe. Hayo yalibainishwa kwenye risala ya wakazi wa wilaya ya Rungwe kwenye hafla ya uzinduzi wa mradi wa majaribio wa kupinga Unyanyasaji wa kijinsia(GBV) iliyosomwa na mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Tukuyu Day Happy Joseph ambapo kwa wilayani hapa shirika la Watereed litaendesha mradi huo kwa kushirikiana na Kikundi cha Huduma Majumbani(Kihumbe). Happy alisema licha ya serikali kwa kushirikiana na wadau wengine kuendesha kampeni mbalimbali za kuelimisha jaamii juu ya kupinga ukatili wa wa kijinsia bado jamii ya wanaRungwe imeendeleza mila ya kuwatakasa wanawake kwa kuwalazimisha kufanya ngono na mwanandugu wa mume kwa madai kuwa ni kumuondolea mwanamke husika mkosi alioachiwa na mume aliyefariki. Alisema tendo hilo limekuwa likiwakwaza sana wanawake kwakuwa licha ya kutopewa nafasi ya kuchagua pia afya zao huwa hatarini kwakuwa ndugu wanaolazimishwa kufanya nao ngono hakuna anayejua afya zao na wengine huwa na maambukizi ya magonjwa mbalimbali ikiwemo virusi vya ukimwi(VVU). Alisema kupitia mradi wa GBV unaofadhiriwa na mfuko wa raisi wa Marekani,wanawake wanaamini ni wakati sasa wa kuondokana na unyanyasaji huo na kuomba waratibu wa mradi huo kujikita zaidi maeneo ya vijijini kulikokithiri kwa unyanyasaji huo. Kupitia risala hiyo pia wakazi wilayani hapa waliahidi kutoa ushirikiano wa kutosha katika kipindi chote cha miezi 18 ya mradi kwakuwa ukatili ambao umekuwa ukifanywa dhidi ya wanawake na watoto ni mkubwa na kwamba sasa hauvumiliki. Akimwakilisha mkuu wa wilaya ya Rungwe Chrispin Meela,mkuu wa chuo cha Magereza cha Kiwira Kamishina Msaidizi Mwandamizi Stanford Ntirundura alisema kaulimbiu GBV ya Amka sasa,Pinga ukatili wa kijinsia,Mabadiliko yanaanza na wewe umekuja sehemu muafaka kutokana na kukithiri kwa vitendo vya ukatili wa kijinsia na watoto wilayani hapa. Ntirundura alisema wilaya hiyo pia bado inakabiliwa na mila za mume kuwa na sauti katika umiliki wa mali zote na ndiyo sababu wanawake na watoto wamebaki kuwa wazalishaji wakubwa wa mazao lakini hawanufaiki na jasho lao kwakuwa mwisho wa siku mume huchukua fedha zote zilizopatikana kutokana na mazao hayo na yeyeye kutumia ajuavyo. Alisema ni wakati kwa wanaRungwe kubadilika kwa kuhakikisha wanatoa taarifa kwa vyombo husika juu ya matukio ya unyanyasaji yanyofanywa na wachache wanaoamini katika mila zisizoendana na wakati kwakuwa ni kandamizi au zinahatarisha maisha ya watu wa kundi jingine.

No comments:

Post a Comment