Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Saturday, July 6, 2013

BANKI YA POSTA YATOA MIFUKO 100 YA SARUJI KUNUSURU WANAFUNZI KATIKA SHULE YA MSINGI UHURU TUNDUMA KUKAA KWENYE VUMBI

BENKI ya posta nchini imetoa msaada wa mifuko 100 ya saruji yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 7.2 kwaajili ya kukamilisha ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa katika shule ya msingi Uhuru iliyopo Tunduma wilayani Momba. Mhasibu wa benki ya posta tawi la Mbeya Felix Mapunda,alimwajkilisha Mkurugenzi Mkuu wa benki hiyo nchini kukabidhi mifuko hiyo jana. Mapunda alisema suala la kujitolea ni moja ya majukumu ya benki hiyo kwa ajili ya kuisadia jamii katika nyanja zote hususani nyanja ya elimu kwa watanzania ikiwa ni njia pia ya kurejesha faida wanayoipata kwa wananchi. Hata hivyo alisema benki hiyo imeshawishika kutoa msaada huo kufuatia kilio cha wakazi wa mtaa wa Uhuru ilipo shule hiyo walichokipeleka kwa uongozi wa benki wakiomba kuongezewa nguvu ili kukamilisha ujenzi kwa wakati. “Wananchi mlifika mkaomba kusaidiwa.Kwakuwa tuliona na ninyi mmeonyesha moyo wa kujitoa kwa kujenga vyumba vya madarasa matatu,tukaona tuna kila sababu ya kuwaongezea nguvu.Ndiyo sababu leo hii tuko hapa na tunawakabidhi kile mlichoomba”.alisema Mapunda. Aliutaka uongozi unaohusika na ujenzi katika shule hiyo kuitumia saruji hiyo kwa malengo yaliyokusudiwa hasa ujenzi wa sakafu kwakuwa madarasa kwa sasa yanatumika yakiwa na vumbi chini. Kwa Upande wake Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, June Mwandambo, alisema msaada huo ni sehemu ya mchango mkubwa kwa shule hiyo ambayo imeanzishwa mwezi april Mwaka huu ikiwa na wanafunzi 175 kuanzia darasa la kwanza hadi la tatu. Aidha mwalimu Mwandambo alisema shule hiyo inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo majengo yake kutokamilishwa kwa kuweka madirisha hali inayowafanya wanafunzi pamoja na walimu kupigwa na baridi kali wakati wote. Alisema kutokana na uhaba wa dawati ambapo hadi sasa zipo 11pekee inawalazimu wanafunzi wengi kukalia tofali wanazoweka kwenye sakafu ya vumbi na kuandikia kwenye magoti. Naye diwani wa kata hiyo ya Tunduma, Frank Mwakajoka, kwa niaba ya wananchi wake aliishukuru benki hiyo kwa kutoa mifuko hiyo ya saruji huku akiihakikishia benki kuwa saruji hiyo itatumika kwa matumizi yanayo kusudiwa na wala si kwa matumizi mengine.

No comments:

Post a Comment