Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, August 6, 2013

ZIARA YA KAMATI YA BUNGE YA HESABU ZA SERIKALI ZA MITAA WILAYANI MBARALI

HALMASHAURI ya wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya imepata wakati mgumu mbele ya kamati ya bunge ya hesabu za serikali za mitaa(LAAC) baada ya kamati hiyo kuutaka uongozi wa halmashauri kueleza sababu ya wao pekee kupata hati chafu katika mwaka wa fedha uliopita. Mwenyekiti wa kamati hiyo Rajab Mohamed Mbarouk aliitaka pia halmashauri kueleza wamejipanga vipi kuahikisha hawakumbwi na dhahma hiyo kwa mara nyingine huku akiwakumbusha kuwa walianza kwa kupata hati ya mashaka,ikafuatia hati safi na mwaka uliofuata waakapata chafu. Maswali hayo ya mwenyekiti na wajumbe wengine watatu yalisababisha mkurugenzi Adam Mgoi na mwenyekiti wa halmashauri hiyo Keneth Ndingo na wataalamu wengi kulazimika kutafuta majibu huku wote wakiwatupia lawama watumishi watano waliofukuzwa kazi hivi karibuni akiwemo mtunza hazina kuwa chanzo cha kupata hati hiyo. “Kwakweli mwenyekiti lazima tuseme ukweli.Mweka hazina aliyekuwepo alikuwa tatizo kubwa na ndiyo sababu tulipobaini mapungufu yake tukaamua kumtimua mapema” alisema Ndingo. Hata hivyo Mwenyekiti wa kamati alionesha kutoridhishwa na majibu hayo na kumwambia Ndingo kuwa walistuka kukiwa kumekucha na pesa za wananchi zikiwa zimekwenda na maji. Hali hiyo ikamlazimu mkurugenzi wa halmashauri Adam Mgoi kuokoa jahazi kwa kueleza mikakati mbalimbali ambayo imewekwa ili kuinusuru halmashauri yao na aibu ya kupata hati chafu. Aliitaja baadhi ya mikakati kuwa ni pamoja na utunzaji sahihi wa kumbukumbu za mapato na matumizi tofauti na awali ambapo zilihifadhiwa kienyeji ama kufichwa wakati wakaguzi walipokwenda kufanya kazi yao. “Kwa sasa tunawahakikishia tunao utaratibu mzuri wa udhibiti wa ndani wa nyaraka zetu.Tumeboresha pia mfumo wa malipo ya ndani.Ili kuhakikisha tunafanya kazi zetu kwa ufasaha tumelazimika kuazima watumishi wawili wa idara ya uhasibu kutoka wilaya jirani ya Chunya ambao tunasaidiana nao kwa sasa”. Alisema mkurugenzi huyo Majibu ya mkurugenzi huyo yalionesha kidogo kuwapa moyo wajumbe wa kamati na mwenyekiti wake kusisitiza kuwa mikakati madhubuti inahitajika kwakuwa ni aibu kubwa kwa halmashauri hiyo kupata hati chafu pekee kati ya halmashauri zote nchini.

No comments:

Post a Comment