Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Monday, August 19, 2013

KANDORO MGENI RASMI MKUTANO WA JUMUIYA YA AHMADIYYA KESHO MBEYA

MKUU wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro kesho(Agosti 20) anataraji kuwa mgeni rasmi kwenye mkutano wa jumuiya ya Waislamu Waahmadiyya wenye lengo la kuzungumza mchango wa dini katika kuleta amani ya taifa na dunia kwa ujumla. Katika kikao chake na waandishi wa habari kiongozi mkuu wa Ahmadiyya nchini Tahir Mahmood Chaudhry amesema mkutano huo utakaoanza majira alasiri utafanyika katika ukumbi wa Mkapa jijini Mbeya. Chaudhry amesema Watendaji kadhaa wa serikali katika ngazi mbalimbali mkoani hapa pamoja na viongozi wa jumuiya za kidini na asasi zisizo za kiserikali wamealikwa kwenye mkutano huo na baadhi yao watapata nafasi ya kuchangia mada hiyo muhimu. Amesema jumuiya hiyo inauona mkutano wa aina hiyo kuwa muhimu hasa katika kipindi hiki ambacho taifa linapita katika wakati mgumu wa mivutano baina ya wanadini wenyewe kwa wenyewe na wakati mwingine na serikali yao. Kiongozi huyo pia amelalamikia mapokeo yasiyo sahihi ya tafsiri za vitabu vitakatifu ikiwemo Kurani kwa baadhi ya wanadini hali aliyosema ni chanzo cha migogoro mingi inayoendelea duniani. Ametaja suala la baadhi ya waumini wa madhehebu ya kiislamu kutumia nguvu na vurugu wakidai ni njia sahihi na kupigania uislamu jambo alilosema si la kweli na kurani haifundishi hayo.

No comments:

Post a Comment