Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Sunday, December 13, 2015

HOSPITALI YA RUFAA KANDA YA MBEYA YAANZISHA NAMBA YA HUDUMA KWA WATEJA

HOSPITALI ya Rufaa kanda ya Mbeya,imetoa namba maalumu za simu za kiganjani zitakazotumika kwaajili ya taarifa za  msaada wa dharula lengo likiwa ni kurahisisha mawasiliano baina ya taasisi hiyo na jamii.

Mkurugenzi wa hospitali hiyo Dk.Mpoki Ulisubisya amesema kwa Makao makuu ya hospitalini hiyo itatumika 0767 314 250 wakati kitengo cha wazazi Meta itatumika namba 0755 333 574.

Anasema kuwekwa kwa huduma ya simu kwaajili ya wateja ni sehemu ya utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa Katibu mkuu wizara ya Afya na ustawi wa jamii Dk.Donan Mmbando alipofanya ziara hospitalini hapo hivi karibuni.

“Sisi tumeona tuanze kutekeleza maagizo tuliyopewa mapema kabisa.Hakuna sababu ya kusubiri tena.Tunahitaji kwenda sambamba na kasi ya uongozi uliopo madarakani ya Hapa kazi tu” anasema Dk.Ulisubisya.

Anasema kuanzisha kwa huduma hiyo kutawezesha ndugu,jamaa na marafiki kupata taarifa sahihi juu ya ndugu zao watakaokuwa wamelazwa kwenye hospitali hiyo kwaajili ya huduma za kimatibabu.

Hata hivyo anasema namba hizo mbili zitatumika kwa muda na ukomo wake utakuwa mara tu baada ya kampuni za simu kutengeneza namba maalumu ambayo mteja wa hospitali atapiga simu pasipo kutozwa gharama zozote.

Alisema tayari uongozi umekwisha wasilisha ombi la kutengenezewa namba hizo maalumu kwenye kampuni moja ya simu na uongozi wa kampuni husima umeridhia kutengeneza namba hiyo.

Kwa upande wao baadhi ya wateja hospitalini hapo wamezungumzia mpango huo kuwa muhimu kwakuwa utawezesha jamii kupata taarifa na majibu sahihi juu ya maswali wanayokuwa wakijiuliza hususani yanapotokea matatizo kama ya ajali na miili ya watu waliopoteza maisha na majeruhi kupelekwa kwenye hospitali hiyo.

No comments:

Post a Comment