Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Wednesday, December 30, 2015

MWILI WA MCHIMBAJI MMOJA WAFUKULIWA KWENYE KIFUSI CHUNYA

JITIHADA za kuokoa wachimbaji wawili waliofukiwa na kifusi katika machimbo bubu ya dhahabu yaliyopo eneo la mnadani kata ya Sangambi, wilayani Chunya zimeendelea tena jana jumanne(Disemba 29) na hatimaye kuzaa matunda kwa mmoja wa wakichamji hao kuopolewa akiwa amefariki dunia. 

Wachimbaji madini hao walifukiwa na kifusi tangu Disemba 27 mwaka huu majira ya asubuhi na shughuli ya kufukua kifusi ili kuwaokoa ikaanza Disemba 28 majira ya asubuhi baada ya mashine ya  kufukua kifusi kupatikana. 

Hata hivyo kutokana na gari lenye mashine hiyo kutokuwa na taa ililazimu shughuli hiyo kusitishwa ilipofika juzi jioni na kiza kuanza kutanda hivyo shughuli hiyo ikaendelea tena jana Disemba 29. 

Akizungumza na Lyamba Lya Mfipa kutoka eneo la tukio,mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Chunya Bosco Mwanginde amesema jitihada za ufukuaji kifusi zilianza kuzaa matunda majira ya saa nane mchana baada ya wananchi waliokuwepo kufanikiwa kuopoa mwili wa mmoja wa wachimbaji hao. 

Mwanginde amemtaja marehemu ambaye mwili wake uliopolewa jana kuwa ni Wambula Makulu mwenyeji wa Musoma mkoani Mara aliyesema alihamia maeneo hayo miaka kadhaa iliyopita.

Mwanginde amesema pamoja na kuukuta mwili huo shughuli ya kufukua kifusi iliendelea kwa lengo la kumtafuta mchimbaji mwingine aliyemtaja kwa jina la Riziki Kalengo mkazi wa wilayani Mbozi japo pia jioni shughuli hiyo ilisimama na imeendelea leo asubuhi.

No comments:

Post a Comment