Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Wednesday, December 9, 2015

KIPINDUPINDU CHAUA WAWILI MBEYA,WENGINE KADHAA TAABANI

Image result for abbas kandoroHOFU ya kusambaa kwa ugonjwa wa Kipindupindu imezidi kutanda mkoani Mbeya licha ya kuwa mkoa huo ni moja kati ya maeneo nchini yaliyoanza kutekeleza mapema agizo la Usafi lililotolewa na Rais John Magufuli.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro amethibitisha kuwepo kwa taarifa za wagonjwa wa kipindupindu katika kambi ya Lema wilayani Kyela.

Kandoro amethibitisha kuwepo kwa ugonjwa huo alipokuwa akiwahamasisha wakazi wa mji mdogo wa Mlowo wilayani Mbozi huku akiwahimiza kuzingatia suala la usafi ili kuepukana na magonjwa ya milipuko kama kipindupindu.

Amesema tayari wagonjwa 27 wa kipindupindu wameripotiwa na wamehifadhiwa katika kambi ya kijiji cha Lema waanakoendelea kupatiwa matibabu lakini tayari wawili kati yao wamefariki.

 “Awali nilidhani mimi nimepona kupata kipindupindu lakini hadi muda huu ninapoongea na nyie nimepata taarifa ya wagonjwa 27 walioko katika kambi ya kijiji cha Lema wilayani Kyela na kati yao wawili wamefariki dunia” anasema Kandoro.

Anasema awali waliripotiwa wagonjwa 9 ambapo kati yao 1 alifariki na wengine 7 walipata matibau na kuruhusiwa kurudi nyumbani huku mmoja akiendelea na matibabu kambini hapo kabla idadi hiyo haijaongezeka.

Amesema njia pekee ya kuepuka ugonjwa huo ni kwa wakazi wa maeneo yote ya mkoa wa Mbeya kuhakikisha wanazingatia usafi huku akisema pamoja na maeneo mengi wananchi kuitikia kwa kasi dhima ya kufanya usafi bado kuna changamoto ya kuwabadili wananchi kuwa na tabia ya kufanya usafi katika mazingira yao.

No comments:

Post a Comment