Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, December 15, 2015

WAKENYA WAKIRI KUMHITAJI DK.MAGUFULI

RAIA wa Kenya na Mkurugenzi wa mkuu wa Kampuni ya BAYLEM limited  ya nchini Kenya John Ogumbo amesema wakenya wanaowaonea wivu Watanzania kwa kupata rais mchapa kazi na mwenye kuonesha uzalendo wa kweli kama ilivyokuwa kwa viongozi waasisi wa mataifa ya barani Afrika.

Ogumbo aliyasema hayo alipoungana na viongozi wa kampuni ya Hamiliton Medical kukabidhi msaada wa Mashine ya msaada wa Kupumulia yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 80 kwa hospitali ya Rufaa kanda ya Mbeya.

Mkurugenzi huyo alisema kwa sasa kinachozungumzwa katika kila kona ya nchi ya Kenya na kwingineko wanakofanya shughuli za usambazaji wa vifaa kwenye hospitali ni utendaji kazi wa Dk.John Magufuli.

Alisema watu wengi wanauona utendaji kazi wa rais huyo kama wa mtu ambaye kamwe hakutarajiwa tena kuja kuonekana katika uongozi wa ulimwengu wa sasa kutokana na viongozi wa mataifa mengi hivi sasa kuwa na utendaji usioendana na matakwa ya wananchi wao.

“Mmepata kiongozi wa ajabu.Kila mkenya anashangaa,tunatamani tungempata sisi.Kwakweli sisi wakenya tunawaonea wivu kwa kupata kiongozi huyu” alisema Ogumbo.

Hata hivyo Ogumbo aliwasihi watanzania kuhakikisha wanamuombea kwakuwa ni jambo lisilopingika kuwa kwa utendaji kazi wake ni wazi atajiongezea maadui tena wale walio na uwezo wa kufanya jambo lolote kutokana na uwezo wao kipesa.

Alisema watanzania pia wanapaswa kumpa ushirikiano wa kutosha akisema kufanya hivyo kutawezesha taifa lao kupata mabadiliko makubwa ya kimaendeleo katika kipindi cha miaka mitano tu na kuifanya Tanzania kuwa nchi ya kuigwa na kila mtu duniani.

Alisema iwapo watanzania watashindwa kuitumia fursa ya uwepo wa Dk.Magufuli kwenye utawala watakuja kujijutia na kamwe hawatokuja tena pata nafasi ya kubadili maisha yao na huenda ukawa mwisho wa kuendesha mashindano ya kimageuzi ya maisha bora na mataifa mengine.

Akizungumzia msaada wa mashine ya kupumulia,alisema kambuni hizo mbili ziliguswa baada ya kutembelea hospitali hiyo hususani katika kitengo cha wazazi Meta na kujionea mashine zinazotumika bado zi za teknolojia ya zamani.

Alisema mashine waliyokabidhi inao uwezo wa kuokoa maisha ya mtoto aliyezaliwa kutoka ujauzito wa miezi mitano na inatumika pia kwa watu wazima walio na uhitaji wa msaada wa upumuaji.

Kwa upande wake Meneja mauzo ukanda wa Afrika wa kampuni ya Hamiliton Medical Gordon Blair aliahidi kuendelezwa kwa mashirikiano yaliyopo baina ya taasisi za afya nchini na kampuni hizo lengo likiwa ni kuwezesha utoaji wa huduma bora za afya kwa jamii.

Naye kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa kanda ya Mbeya Thomas Isdory alisema msaada huo utasaidia kupambana na changamoto ya vifaa tiba huku akisema mashine za aina hiyo zinahitajika zaidi kutokana na mwenendo wa utoaji huduma kwenye hospitali hiyo.

No comments:

Post a Comment