Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Wednesday, December 30, 2015

WATATU MBARONI KWA KUMUOZESHA BINTI KWA KIKONGWE



DAWATI la jinsia na watoto la jeshi la polisi wilayani Nkasi mkoani Rukwa linawashikiliwa watu watatu wakazi wa kijiji cha mkole kwa kosa la kumlazimisha mtoto wao wa kike wa miaka 18 kuolewa na Mwanaume wa miaka 72 baada ya kutoa mahali ya ng’ombe 8 na shilingi 100,000.

Akizungumza binti huyo( Jina linahifadhiwa) mbele ya dawati hilo alisema kuwa wazazi wake walichukua mali kwa mzee Edward Muscat (72) Ng’ombe 8 Tshs,100,000 bila kumshirikisha na kuamua kumlazimisha kwenda kuolewa na mzee huyo ambaye kiuhalisia ni Babu yake.

Alisema kuwa yeye baada ya kuambiwa na wazazi wake ya kuwa akaolewe na mzee huyo alikataa na ndipo walipomlazimisha kwenda kwa nguvu kwa mzee huyo ambapo aliishi naye kindoa kwa muda wa siku Nne na ndipo alipotoroka na kukimbilia polisi.

Alisema yeye kila akirudi nyumbani wazazi wake hao umfukuza na kumalazimisha mtoto huyo kwenda kwa mmewe huyo kwa madai kuwa walishapokea mali hivyo ni lazima aolewe na mzee huyo.

Baba wa mtoto huyo Mboje Saguda baada ya kumhoji juu ya tukio hilo akiwa mikononi mwa polisi sambamba na mkewe alikiri kupokea mali hiyo kutoka kwa mzee huyo na kuwa wao hiyo kwao ni mila wala siyo tatizo.

Na alidai kuwa mtoto wao huyo licha ya kukataa kuolewa na mwanaume huyo ilikua ni lazima aolewe ili kukidhi matakwa ya mila yao ya kabila la Wasukuma.

Mwenyekiti wa dawati la jinsia na watoto wa wilaya Nkasi Anna Kisimba alisema wazee hao wamekwenda kinyume na haki za binadamu na kuwa hivyo ni vitendo vya kikatili dhidi ya mtoto wa kike na kuwa hivi sasa wanaandaa mashitaka ya kuwafikisha mahakamani watuhumiwa wote watatu ya kumdhalilisha mtoto wa kike.

Alisema wazee hao mume na mke ikiwa ni pamoja na muoaji wametenda kosa la jinai kumlazimisha binti mdogo kuolewa na Babu kwa lazima,na kuwa licha ya kwamba binti huyo kwa umri aliofikia ni halai kuolewa lakini si katika mazingira ya kulazimishwa kwa tamaa ya mali na kuwa suala la kuoa ama kuolewa ni la hiari hivyo ni lazima kila mmoja akubali kwa dhati kutoka moyoni mwake.

Mkuu wa polisi ( OCD) wilayani Nkasi Cyprian Mushi alikiri jeshi lake kuwashikilia watu hao kwa maana wazazi wa binti na muoaji kwa kwenda kinyume na haki za binadamu na kuwa ni kitu ambacho hakikuballiki kuoana kwa kutofautiana umri kwa mbali kiasi hicho hata kama wamekubaliana.

Amesema kuwa kosa kubwa kwa watuhumiwa hao ni kitendo cha kumlazimisha binti ambaye kimsingi ana maamuzi yake na hilo lote ni shinikizo litokanalo na tamaa ya mali iliyopelekea kumdhalilisha binti huyo kijinsia,na kuwa upelelezi umekamilika kuanzia sasa watafikishwa mahakamani kujibu yuhuma hizo.

Na Israel Mwaisaka,Nkasi

No comments:

Post a Comment