Uongozi wa Yanga, umetangaza kuvunja mkataba
wake na kiungo wake Haruna Niyonzima.
Yanga imechukua uamuzi huo ikiwa ni miezi
isiyozidi mitano tokea isaidi mkataba mpya wa miaka miwili na Niyonzima.
Msemaji wa Yanga, Jerry Muro amesema
Niyonzima atalazimika kulipa kiasi cha dola 71,175 (zaidi ya Sh milioni 149)
kutokana na kukiuka mkataba uliosababisha kuvunjika kwa mkataba huo.
Mzozo wa Yanga na Niyonzima ulianza baada ya
kiungo huyo kuchelewa kurejea kazini alipokwenda kuitumikia timu yake katika
michuano ya Chalenji nchini Ethiopia.
Uongozi wa Yanga ulimsimamisha kwa madai
amekuwa na tabia hiyo ya kuchelewa kila mara na kumtaka atoe maelezo.
No comments:
Post a Comment