Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Saturday, June 1, 2013

MADIWANI WA CHADEMA WAGOMA MKOA WA MBEYA KUGAWANYWA

kWAKATI mchakato wa kuugawa mkoa wa Mbeya ukiendelea kwa wadau mbalimbali wakiwemo madiwani kutoa maoni yao kabla ya kufanyika kwa kikao cha Ushauri cha mkoa(RCC) madiwani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema) katika halmashauri ya jiji wameibuka naa jambo jipya. Madiwani hao walionesha utofauti kwenye kikao cha balaza la madiwani kilichofanyika jana ambapo kila madiwani wa chama kimoja walipaswa kuwasilisha maoni yao ya namna ya kuugawa mkoa,jina la mkoa mpya,wilaya zinazopaswa kuzalishwa kutokana na mgawanyo huo pamoja na makao makuu ya mkoa mpya. Kikiwa inakaribia kumalizika ndipo katibu wa balaza hilo kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya jiji Dk.Samwel Lazaro alisema maoni yaliyowasilishwa na madiwani wa Chadema ni kuwa hawaoni sababu ya kuugawa mkoa wa Mbeya. Kwa mujibu wa Dk.Lazaro madiwani hao waanaona kuugawa mkoa wa Mbeya ni mbinu inayotumiwa na viongozi wa serikali ya Chama Cha Mapinduzi kugawana madaraka ya kiutawala. Pia alisema walieleza kufanya hivyo ni kuwapa mzigo mkubwa wananchi wa kugharamia malipo ya mishahara na matumizi mingine katika ofisi hizo mpya za mikoa na wilaya. “Katika maoni yao wao wamesema badala ya rais kuugawa mkoa wa Mbeya na kuwa mikoa miwili ni vema akatoa fursa hiyo kwa majimbo yaliyo makubwa yaweze kugawanywa.Wao wanaamini kugawa majimbo ni njia sahihi ya kuwasaidia wananchi” Hata hivyo maoni ya madiwani hao yalionekana kupokelewa kwa hisia tofauti na wajumbe wengine wa kikao hicho hususani madiwani wa CCM na NCCR Mageuzi ambao walilazimika kuonesha mshangao mkubwa na kuwaona wenzao kaama miongoni mwa wadau wasioutakia maendeleo mkoa wao. Akizungumzia maoni hayo meya wa jiji hilo Athanas Kapunga alisema ni jambo la kushangaza kwa watu wanaotambua fika ukubwa wa mkoa wa Mbeya unaoongoza kati ya mikoa yote nchini wakanzisha hoja ya kupinga kuugawanya. Alisisitiza kuwepo na umuhimu mkubwa wa kuugawa mkoa wa Mbeya akisema kutasaidia kuboresha huduma za kijamii sambamba na kukuza demokrasia kwa wananchi. Aliwasihi wakazi wa jiji la Mbeya na mkoa kwa ujumla kutokubali kupotoshwa na wanasiasa walio na misimamo isiyolenga kujenga bali walione wazo la rais kama busara aliyoamua kuitumia kuwarahisishia kupata maendeleo. Kwa upande wa madiwani wa NCCR walipendekeza mkoa ugawanywe na kupatikana mkoa mpya wa Kiwira utakaoundwa na wilaya za Rungwe,Kyela,Ileje,Busokelo na Mbarali na maakao makuu yawe Tukuyu wilayani Rungwe na wilaya zinazosalia zibaki mkoa wa Mbeya.

No comments:

Post a Comment