Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, June 28, 2013

VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA RUNGWE WATAKA KUPEWA MKOA MPYA,MADIWANI NAO WATOA JENGO JIPYA LA HALMASHAURI LITUMIKE KAMA OFISI ZA MKOA MPYA IWAPO WATAKUBALIWA

VIONGOZI wa vyama mbalimbali vya siasa wilayani Rungwe wamezungumzia umuhimu wa kuugawa mkoa wa Mbeya huku wote wakionekana mkoa mpya kuitwa jina la wilaya hiyo na makao makuu kuwa mjini Tukuyu. Katika maeneo na nyakati tofauti viongozi hao wameiambia Tripe A kuwa kutokana na historia kuonyesha Rungwe kuwa wilaya ya muda mrefu iliyowezesha kupatikana kwa wilaya nyingine za mkoa wa Mbeya kuna haja ya mkoa mpya kupeleletwa wilayani hapa. Katibu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) wilayani hapa Ramadhan Sevungi alisema ni muhimu mkoa mpya ukaitwa Rungwe na wilaya ya Rungwe kwa sasa ikabadilishwa jina na kuitwa wilaya ya Tukuyu. Sevungi alipendekeza halmashauri ya Busokelo iliyoanzishwa hivi karibuni kupewa wilaya ili iweze kuungana na wilaya za Kyela,Ileje,Tukuyu itakayounganisha na baadhi ya maeneo ya wilaya ya Mbeya kuunda mkoa wa Rungwe. Ka upande wake Katibu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema) wilayani hapa Antony Mwasasungura alisema kutokana na historian a umaarufu wa watu wa kabila la Wanyakyusa ambao chimuko lao ni wilaya ya Rungwe mkoa wa Mbeya umekuwa na umaarufu mkubwa katika Nyanja za kisiasa na uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara hivyo ni vema ukanda huo ukapewa heshima ya kuwa mkoa. Mwasasungura alisema kwa kupewa mkoa wakazi wa ukanda huo ambao wengi ni wakulima wataweza kuneemeka kupitia fursa za ajira zitakazopatikana kutokana na uwepo wa viwanda hususani vya kusindika matunda kwakuwa kutakuwa na msukumo wa karibu wa kuhamasisha uwekezaji. Naye mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi(CUF) Antony Mwaihojo aliitaja Rungwe kuwa moja ya wilaya zilizo na rasilimali nyingi zinazotosha kujiendesha hata ikipewa hadhi ya kuwa mkoa. “Wilaya yetu ina kanda tatu,Tuna uwanda wa juu wa baridi,uwanda wa kati na ule wa joto.Hizi zote ni fursa zinazotuwezesha kulima mazao ya aina zote na kwa misimu yote ya mwaka.Hivyo tunao uwezo wa kuzalisha mazao ya chakula na biashara yanayoweza kutuingizia kipato na pia akiba ya kutosha ya chakula”

No comments:

Post a Comment