Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Saturday, December 21, 2013

MADIWANI WATAKA TAARIFA YA MAUZO YA JEZI ZA MBEYA CITY

MADIWANI wa halmashauri ya jiji la Mbeya wameagiza taarifa za mapato na matumizi ya fedha zitokanazo na mauzo ya jezi za timu ya Mbeya City kuwekwa wazi. Madiwani walitoa agizo hilo jana kwenye kikao cha kawaida cha balaza la madiwani wa halmashauri hiyo kilichofanyika kwenye ukumbi wa halmashauri eneo la uhindini. Madiwani hao walisema wamekuwa wakishuhudia jezi za Mbeya City zikiagizwa kutoka nje ya nchi na kuuzwa katika maeneo mbalimbali lakini hawajui fedha zinazopatikana zimekuwa zikitumika namna gani. Mmoja wa madiwani hao Frank Mayemba kutoka kata ya Itezi alisema kwakuwa timu ni mali ya wananchi kupitia Halmashauri yao ni lazima wananchi wapewe taarifa ya mapato ya fedha zitokanazo na mauzo ya jezi. “Jezi zina nembo ya halmashauri hivyo ni sehemu ya vyanzo vya mapato vya halmashauri yetu.Sasa tunapokuwa hatupewe taarifa kuwa halmashauri inmenufaika namna gani kwa kuuza jezi wananchi wanakuwa hawatendewi haki.Lazima tupewe taarifa ya mauzo ya jezi ili tubaini kama kuna ufisadi unaofanyika au la” alisisitiza Mayemba. Alisema balaza kupitia vikao vyake limekuwa likiishia kupewa taarifa za mishahara ya makocha,wachezaji na viongozi wengine wa timu lakini hakuna siku taarifa za mauzo ya jezi zimetolewa. Hata hivyo diwani huyo alisema huenda kasoro ya kutowekwa wazi kwa taarifa za fedha zitokanazo na mauzo ya jezi pamoja na michango ya wadau inatokana na mfumo wa muundo wa uendeshaji wa timu chini ya bodi hali aliyosema mfumo huo unapaswa kutazamwa upya. Kwa upande wake mstahiki Meya wa jiji la Mbeya Athanas Kapunga,aliahidi taarifa za mapato yatokanayo na mauzo ya jezi pamoja na michango kutoka kwa wadau kuletwa katika kikao kijacho cha balaza hilo.

No comments:

Post a Comment