Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, December 20, 2013

MAUAJI YA KUTISHA YAFANYIKA NYUMBANI KWA DIWANI WA CCM

MAUAJI ya kinyama yamefanyika nyumbani kwa diwani wa kata ya Nkangamo wilayani Momba(CCM) baada ya mwanaye na mfanyakazi wa ndani kuuawa kikatili na watu wasiofahamika. Diwani aliyekumbwa na maswahibu hayo ametajwa kwa jina la Eston Kimwelu(55) mkazi wa mtaa wa Tazara katika mji mdogo wa Tunduma wilayani Momba ambapo mauaji hayo yalitokea Desemba 19 mwaka huu saa 8:00 mchana nyumbani kwake. Kaimu kamanda wa polisi mkoani Mbeya Barakael Masaki amewataja waliouawa katika tukio hilo kuwa ni mtoto wa diwani huyo Kalibu Kimwelu(6) aliyeuawa kwa kuchinjwa shingo kwa kisu wakati mfanyakazi wa ndani Sista Nyilenda(17) aliuawa kwa kunyongwa shingo kwa kutumia waya wa Luninga uliopo katika sebule ya nyumba ya familia hiyo. Masaki amesema wakati mauaji hayo yakitokea diwani Kimwelu alikuwa shambani kwake katika kijiji cha Kipaka huku mkewe Tumaini Yohana(29) katibu muhtasi wa halmashauri ya mji mdogo wa Tunduma wilayani hapa akiwa kazini. Amesema miili ya marehemu wote wawili ilikutwa katika sebule ya nyumba hiyo lakini pia bada ya kuchunguza ikabainika wauaji waliiba mabegi mawili yenye nguo yaliyokuwa katika chumba wanacholala watoto. Kaimu kamanda huyo amesema chanzo cha mauaji hayo bado kinachunguzwa ijapokuwa kinahusisha na mgogoro wa muda mrefu wa kifamilia baina ya mke mdogo na mkubwa ambapo familia ya mke mkubwa imekuwa ikidai kutelekezwa na mumewe kwa kunyimwa mali yakiwemo mashamba. Kufuatia tukio hilo jeshi la polisi linawashikilia watu watano wakiwemo watoto watatu wa mke mkubwa aliowataja kwa majina ya Enock(23) ,Gabriel(19) na Alex(16) na marafiki wa familia hiyo Mussa Ngoba(19) na Patrick Msigwa(18).

No comments:

Post a Comment