Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Sunday, December 15, 2013

WADAU WAJITOKEZA KUSHIRIKI KAMPENI YA SHARING IS MORE THAN GIVING

Mhariri mkuu wa Lyamba Lya Mfipa Bwana Joachim Nyambo(wa tatu kulia)akiwa na wanakikundi wa PMM GROUP alipotembelea kwenye viwanja vya Youth Centre linakofanyika zoezi la kupokea michango mbalimbali kupitia kampeni ya Sharing is more than Giving itakayopelekwa katika vituo vya watoto yatima na pia magerezani kwaajili ya wafungwa. Baadhi ya vitu vilivyokusanywa kutoka kwa wadau mbalimbali walioguswa na kampeni hii WAKAZI jijini Mbeya wamezidi kujitokeza katika viwanja vya ukumbi wa Youth Centre jijini hapa kushiriki katika kampeni ya Sharing is more than Giving kwa kupeleka vitu mbalimbali ikiwemo nguo na vyakula. Muungano wa PMM unaojumuisha Taasisi ya kuelimisha umma dhidi ya kupinga ugaidi na Maendeleo(PTA & HW trust Fund),Miss Mbeya 2013 Jacklin Luvanda na Maisha Group ndio ulioandaa kampeni hiyo ukilenga kukusanya na kisha kupeleza zawadi hizo kwa makundi yenye mahitaji ikiwemo watoto yatima na wafungwa magerezani. Baadhi ya vitu ambavyo vimewawasilishwa kwa waratibu wanaoendelea kupokea katika viwanja hivyo ni pamoja na sukari,nguo mbalimbali kwaajili ya mavazi na malazi,sabuni na fedha taslimu. Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya kampeni hiyo na pia katibu wa PTA Arthur Kasiba amesema walifikia uamuzi huo baada ya kutembelea baadhi ya vituo vya kulelea watoto yatima na pia magerezani na kukuta jamii iliyopo huko inahitaji msaada wa hali na mali. Amewapongeza wadau mbalimbali wanaoendelea kujitokeza kuchangia kwa kadiri wanavyoweza na kutoa mwito kwa wengine kuzidi kuichangia jamii iliyo na mahitaji kutokana na kuwa katika mazingira mahumu. Jumapili hii jioni ndipo idadi ya vitu vilivyokusanywa itatangazwa katika hafla fupi itakayofanyika GR Hotel na pia vituo ambavyo misaada hiyo itapelekwa.Ikumbukwe kuwa mdau unaweza kuchangia hata nguo unayoona hauwezi kuivaa pengine kwakuwa inakubana au una nyingine na hivyo hauana haja ya kuilundika ndani.Tuungani kusaidia jamii zenye uhitaji

No comments:

Post a Comment