Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Thursday, May 17, 2012

JIULIZENI MMEFANYA NINI NDIPO MUULIZE VIONGOZI WAMEFANYA NINI

MWITO umetolewa kwa wakazi wilayani hapa kuhakikisha wanatambua kuwa uwajibikaji unaopaswa kuhojiwa si kwa upande wa viongozi pekee bali pande zote ikiwamo wao.

Hayo yameelezwa na katibu tawala wa wilaya hiyo Josephat Kakuru alipokuwa akifungua mdahalo wenye lengo la kuimarisha uwazi,uwajibikaji na uhusiano baina ya viongozi waliochaguliwa na wananchi uliaondaliwa na mtandao wa asasi zisizo za kiserikali wilayani Nkasi(NKANGONET)na kufanyika katika kata ya Kirando.

 Kakuru amesema watu wengi wamekuwa wakihoji juu ya uwajibikaji wa viongozi pekee na kutoa malalamiko mengi wakiwalenga viongozi wanaoonekana kutowajibika ipasavyo wakisema wanakwamisha maendeleo yao.


Kwa upande wake mbunge wa Nkasi kaskazini Ally Kessy alikiri kuwepo kwa watu wengi wanaopenda kuhoji utekelezaji wa majukumu ya viongozi wao lakini wao hujitoa ni kama si sehemu ya kumsaidia kiongozi akatimiza wajibu wake.

Kessy ametolea mfano kwa vitendo vya wizi wa fedha za serikali vinavyofanywa na baadhi ya maafisa wa mamlaka ya mapato TRA na mabwana samaki katika mwambao wa ziwa Tanganyika akisema licha ya wananchi kushuhudia uozo unaofanywa bado hawatoi taarifa mahali popote.

No comments:

Post a Comment