Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, May 25, 2012

WAJASIRIAMALI MBARALI WAFUNDWA


WAJASIRIAMALI wilayani Mbarali wametakiwa kufanya shughuli zao kwa misingi inayotarajiwa kubadilisha muonekano wao kutoka walipo na kupiga hatua zaidi kimaendeleo.

Kaimu mkuu wa wilaya ya Mbarali Moses Mashala ameyasema hayo wakati akifunga mafunzo ya siku nne ya wajasiriamali wilayani humo yaliyoandaliwa na chama cha wafanyabiashara,wenye viwanda na wakulima(TCCIA) mkoa wa Mbeya.

Bwana Mashala amesema lengo la serikali pamoja na wadau wengine ni kuona kunakuwepo na mabadiliko katika shughuli za kibiashara zinazofanywa na wajasiriamali nchini hivyo ni changamoto kwa kila anayepata fursa ya kupewa mafunzo kama hayo.

Naye mwenyekiti wa TCCIA mkoani humo Julius Kaijege alisema lengo la mafunzo hayo ni kuwawezesha vijana na waanawake kuondokana na makundi yanayohatarisha maisha yao kwa kujikita katika ujasiriamali.

Mafunzo hayo yaliyoshirikisha jumla ya wajasiriamali 45 yalilenga utengenezaji wa bidhaa mbalimbali ikiwemo mishumaa pamoja na sabuni.

No comments:

Post a Comment