MKUU wa wilaya ya Mbozi
Gabriel Kimolo ametangaza kujiudhuru wadhifa huo kutokana na sababu tatu
alizozitaja kuwa kikwazo kikubwa katika utendaji kazi wake.
Kimolo alitangaza uamuzi huo Mei 4,2012 katika kikao chake na waandishi wa habari kilichofanyika katika
hoteli ya Beaco iliyopo Forest
mpya jijini Mbeya.
Alisema mpaka anzungumza na
wanahabari alikuwa amekwishamwandikia barua rais kumweleza nia hiyo na nakala
ya barua hiyo kuipeleka kwa mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro,ofisi ya waziri
mkuu na ofisi ya waziri wa tawala za mikoa na serikali za mikoa(Tamisemi).
Akielezea sababu za kujiuzuru
kwake alitaja sababu ya kwanza kuwa ni kutoteuliwa upya kwa wakuu wa wilaya
tangu mkataba wao wa kazi ulipomalizika baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010.
Alisema hatua hiyo
imewasababishia kuendelea kufanya kazi pasipo mpango mkakati kwakuwa hawajui
lolote linaloendele juu yao
hivyo kujikuta wakiishia kufanya shughuli zao kwa zima moto.
Alisema kwa kufanya hivyo
hakuweza kuwatumikia wananchi wa wilaya hiyo na kuona kama
mtu asiyestahili kuendelea kuwa kiongozi wao huku akiongeza kuwa hali hiyo pia
imemuathiri yeye na familia yake kwa kiasi kikubwa kwakuwa alilazimika
kusimamisha mipango yake yote.
Kimolo aliitaja sababu ya
pili iliyopelekea uamuzi huo kuwa ni ukumbatiaji wa vitendo vya kifisadi
kunakofanywa na baadhi ya viongozi wa serikali ambao umekuwa tatizo kubwa
katika utendaji kazi wake.
“Sababu hii inatokana na hali
halisi iliyopo wilayani Mbozi juu ya biashara ya kahawa mbichi ambapo licha
serikali ya wilaya na mkoa kuweka msimamo wa kutoruhusu ununuzi wa kahawa
mbichi inaonekana wizara bado inatoa vibali vya ununuzi huo bila kujali kuwa
wananchi wanaumia” alisema
Alisema suluhisho la mgogoro
wa ununuzi wa kahawa mbichi limeendelea kuwa kitendawili kwakuwa licha ya
viongozi wa wizara waziri Profesa Jumanne Maghembe na naibu wake Christopher
Chiza kufika wilayani hapo bado walikuwa na majibu yasiyoridhisha na kuonesha
dhahiri kuwa maamuzi ya wilaya na mkoa hawaridhiki nayo.
“Ni dhahiri kuwa uongozi wa
wizara ndiyo unayoyapa makampuni kiburi cha kuendelea kuwaumiza wananchi kwa
kuwaibia kupitia ununuzi wa kahawa yao
mbichi na waoa kupata faida kubwa mno.Ni kutokana na kinga hiyo wenye makampuni
wanafikia hatua ya kututukana wakisema hawazungumzi na mbwa bali mfuga mbwa”
aliongeza.
Aliitaja sababu ya tatu kuwa
ni hali ya wizi na ucheleweshaji wa pembejeo za ruzuku zinazotolewa na serikali
kwaajili ya kuwasaidia wakulima wadogo ambapo kwa wilaya yake malalamiko
yamekuwa makubwa hali inayowashushia hadhi viongozi wa halmashauri na wilaya
kwa uozo uliofanywa na uongozi wa wizara.
No comments:
Post a Comment