Tamko
la Mwanjelwa alilolitoa kwa waandishi wa habari leo(Mei 7) na gazeti moja la
hapa nchini kumkariri kuwa ana niaa ya kukihama chama chake kutokana na rais
Jakaya Kikwete kuteua wabunge ndani ya muda mfupi na kuwapaa nafasi ya uwaziri.
Gazeti
hilo lilimkariri mbunge huyo ambaye ndiye kipindi chake cha kwanza kuwa
miongoni mwa wabunge wa bunge la Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania akisema
uteuzi wa rais Kikwete kwa mawaziri haukumridhisha kwakuwa wapo wabunge akiwemo
yeye waliopaswa kupewa wadhfa huo kwakuwa wabunge wa muda mrefu.
Lakini
Mwanjelwa anakanusha kuzungumzia suala la yeye kuhama na kusisitiza kuwa habari
zilizoandikwa si za kweli na kulitaka gazeti lililochapisha habari hiyo kuomba
radhi kabla hajachukua hatua za kisheria dhidi ya mwandishi wa habari hizo
pamoja na kampuni husika.
No comments:
Post a Comment