Wadau hao walitoa malalamiko hayo walipo kuwa
wakizungumza kwa nyakati tofauti na
waandishi wa habari walikuwa katika mafunzo ya habari za uchunguzi jijini Mbeya
yaliyoandaliwa na Umoja wa klabu za waandishi wa habari nchini(UTPC) chini ya
uratibu wa Chama cha waandishi wa habari mkoani hapa(MBPC).
Walionesha kushangazwa na hatua ya halmashauri
kukarabati barabara mara kwa mara kwa
kutumia udongo hali ambayo imekuwa ikichangia kuwepo kwa usumbufu kwa watuiaji hao.
Walifafanua kuwa
katika kipindi cha mwenzi Januari hadi Mei barabara hiyo imefanyiwa
ukarabati mara nne kwa kutumia
udongo jambo linalowakera na kuda kuwa
ni ufujaji wa fedha za umma.
Mmoja wa watumiaji wa barabara ambaye ni dereva tax
Patrick Mbilikile alisema hali ya barabara
hiyo kwa sasa ni mbaya na kuwasababishia gharama za matengenezo ya mara kwa mara ya
magari yao.
“Nashindwa
kuielewa serikali yangu japo imenikuza lakini mambo inayoyafanya kutokana na
kodi zetu hayalengi kutuletea maendeleo.Sijawahi kuona bara bara ya lami
inakarabatiwa kwa kuwekwa udongo sasa halmashauri yetu tangu mwaka jana
inafanya ukarabati wa aina hii na
kusababisha bara bara isidumu hali hii inatupa hasara kubwa sisi ambao magari
yetu yanaharibika mara kwa mara”alisema Mbilikile.
“Tunauliza kama ushuru wa maegesho tunalipa na
kodi nyingine zote sasa kwanini
halmashauri isijipange ikajenga bara bara hii upya badala ya kuendelea kuijaza
udongo”aliongeza.
Mmoja wa Madereva wa dala dala zinazotoa huduma za
usafiri Jijini hapa Castor Mwambembela alisema kuwa
kinachofanywa na halmashauri kwa bara bara hiyo ni sawa na utani kwani licha ya ukarabari wa namna hiyo kufanyika
mwaka jana kwa vipindi tofauti na kuonyesha kutokuwa na ufanisi bado inaendelea
na ukarabati wa aina hiyo.
Aliongeza kuwa katika ukarabati wa mwaka jana kuna wakati walijaribu kutumia Zege
iliyochanganywa na Saruji katika kuziba vilaka lakini bado haikuweza kudumu
hivyo fedha za walipa kodi kuendelea kupotea pasipo mabadiliko yeyote.
Kwa upande wake abiria wa daladala Christina Ikusya
alisema bara bara zilizopo jijini Mbeya
hazivutii hivyo ni changamoto kwa halmashauri kujipanga na kuhakikisha
inazijenga katika kiwango kinachoendana na hadhi ya Jiji.
Aidha waandishi wa habari walishuhudia
ukarabati ukiendelea kwa kutumia udongo
ambapo mafundi waliokuwa wakiendelea na kazi hiyo walipohojiwa kuhusu
ukarabati, walisema wanafanya hivyo ili kuziba mashimo kuondoa usumbufu kwa watumiaji wa barabara
wakati matengenezo makubvwa
yakisubiriwa.
Mmoja wa wafanyakazi hao ambaye alikataa kutaja jina
lake kwa madai kuwa yeye si msemaji alibainisha kuwa barabara hiyo inatarajiwa
kufanyiwa ukarabati mkubwa kwa kiwango cha lami hivi karibuni, ingawa hakutaja
ni lini.
Hata hivyo juhudi za kumpata Mkurugenzi wa jiji
kuzungumzia suala hilo hazikuzaa matunda`baada ya kumkosa ofisini kwake na
alipotafutwa kwa njia ya simu yake ya kiganjani
alijubu kwa ujumbe mfupi kuwa yupo kwenye kikao na kuwa atapiga simu
mara baada ya kikao.
Mwisho
No comments:
Post a Comment