Mamuzi huo ulitolewa leo na Majaji watatu
waliokuwa wakisikiliza kesi hiyo chini ya Mwenyekiti wao Jaji Januari
Msofee ambao ni Jaji William Mandia na Jaji Mbarouk S.Mbarouk baada ya Wakili wa
mlalamikaji Victor Mkumbe kuwakilisha ombi la kutaka kuondoa shauri hilo mahakamani hapo.
Akiwasilisha ombi hilo mbele ya mahakama hiyo ya rufaa wakili
Mkumbe amesema kuwa amefikia uamuzi huo baada ya mlalamikaji kuonyesha nia ya
kutotaka kuendelea na kesi hiyo
Baada ya maelezo hayo jaji Msofee amemhoji wakili wa
mlalamikiwa Benjamini Mwakagamba kama angekuwa na la kusema baada ya kusikia
ombi la mlalamikaji naye akakubaliana na ombi hilo lakini akiitaka mahakama kumwamuru
mlalamikaji kumlipa gharama alizotumia.
No comments:
Post a Comment