WAHAMIAJI
haramu sita raia wa Ethiopia wamefariki dunia na wengine 13 kujeruhiwa baada ya
gari waliyokuwa wakisafiria kutumbukia mtoni.
Msemaji
wa jeshi la polisi mkoani Mbeya Mbogela Majaliwa amesema ajali hiyo imetokea
Mei 7 mwaka huu majira ya saa 4:30 usiku katika mto Lutete uliopo kijijini
Luswiswi tarafa ya Bundali wilayani Ileje.
Majaliwa
amesema wahabeshi hao wakiwa jumla 67 wote wanaume walikuwa wakitokea Tanga na
lengo likiwa ni kwenda Afrika kusini kupitia nchi jirani ya Malawi kwa kutumia
gari lenye namba T 934 AAR Mitsubish Fuso mali ya Mandali Msuya.
Amewataja
waliofariki dunia na kutambuliwa kuwa ni Lamasa Lamole na wawili walio
tambuliwa kwa jina moja moja ambao ni Tamlat na Ibrahim na wengine watatu bado
hawajatambuliwa na miili ya marehemu wote imehifadhiwa katika hospitali ya
wilaya ya Ileje.
Kwa
upande wa majeruhi,kumi wamelazwa katika hospitali ya misheni Isoko na watatu
kwenye hospitali ya wilaya huku wengine 48 walionusurika wakiendelea
kushikiliwa katika kituo cha polisi cha wilaya ya Ileje na Dereva ambaye bado
hajafahamika alikimbia baada ya tukio.
No comments:
Post a Comment