Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, May 29, 2012

MAANDALIZI UMISETA MBEYA YAIVA


TIMU shiriki za mashindano ya michezo mbalimbali kwa shule za Sekondari (UMISETA) mkoani hapa jumatano hii jioni zitaingia kambini tayari kwa mashindano hayo yatakayoanza kimkoa Mei 31 mwaka huu.

Afisa michezo mkoa wa Mbeya George Mbijima ameiambia LYAMBA LYA MFIPA kuwa mashindano hayo yataendeshwa kwa muda wa siku nne katika viwanja vya shule ya sekondari Iyunga jijini Mbeya na yatashirikisha timu kutoka halmashauri nane zilizopo mkoani hapa.

Mbijima amesema mashindano hayo pia yatalenga kuchagua wachezaji wa timu itakayouwakilisha mkoa katika mashindano ya Umiseta kanda ya nyanda za juu kusini yatakayofanyika mjini Sumbawanga mkoani Rukwa.

Ameitaja baadhi ya michezo katika mashindano kuwa ni mpira wa miguu na mkono,wavu,riadha,kikapu,mpira wa meza ma bao yote hiyo ikiwa ni kwa wavulana na wasichana pamoja na mchezo wa netibal kwa wasichana pekee.

Afisa michezo huyo amesisitiza kuwa wachezaji wa timu shiriki ni lazima wawe wanafunzi katika shule za sekondari walio katika utaratibu maalumu unatambuliwa na serikali na si mamluki kutoka mitaani,vituo vya elimu binafsi wala wanaojiandaa kurudia mitihani ya kitaifa ya kidato cha nne au cha sita.

Aidha,ametoa wito kwa wazazi na walimu kuwaruhusu watoto ama wanafunzi wao kushiriki mashindano hayo kwakuwa hiyo pia ni fursa ya wao kuonesha vipaji walivyonavyo na pia kwa kuzingatia umuhimu wa michezo katika afya za miili yao.

No comments:

Post a Comment