Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Saturday, May 5, 2012

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Ndugu Abbas Kandoro ametolea ufafanuzi suala la kujiuzuru kwa aliye kuwa Mkuu wa wilaya ya Mbozi Ndugu  Gabriel Kimolo .
          Akizungumza na waandishi wa habari ofisi kwakwe  Kandoro amesema hadi sasa Rais Jakaya Kikwete hajateua wakuu wa wilaya nchini kwa sababu ambazo zipo ndani ya uwezo wake mwenyewe na yeye hawezi kuzielewa.
 
Amesema siyo kweli kuwa Kimolo amejiuzuru, kwani tayari alikuwa na taarifa kuwa hawezi kuteuliwa kuendelea na wadhifa huo tangu Machi 23, mwaka huu, hivyo aache kutoa visingizio visivyo na mashiko.

Ameongeza mara kuwa baada ya kupewa taarifa za kutoteuliwa tena, Machi 24, mwaka huu Kimolo alimfuata Mkuu wa mkoa ofisini kwake na kulalamika kuwa amefanya kazi kwa uaminifu na uadirifu hivyo ameuamia kwa kupewa taarifa za kutoteuliwa tena.
 
Kwa mujibu wa Kandoro, barua hiyo ya Kimolo ambayo ameipata leo (jana), asubuhi ataifikisha kwenye mamlaka ya utumishi, lakini akamshauri Kimolo ni heri angeondoka kwa amani na siyo kuanza kutoa visingizio visivyo na msingi.
 
Mkuu wa mkoa amesema, ameona ni vyema aliweke wazi jambo hilo kwa vyombo vya habari ili yeyote anayetaka kujiuzuru basi afanye hivyo kwa nia njema na siyo kuwachafua wengine.
 
Wakati huo huo, Kandoro ameweka wazi nia yake ya kumfikisha mwandishi wa habari wa Tanzania Daima, aliyeandika katika gazeti hilo la Machi 5, mwaka huu kuwa Kimolo amesema amefikia adhma hiyo kwa kukosa ushirikiano na Wizara ya Kilimo pamoja na yeye.
 
Ameeleza kuwa  waandishi wa habari ni mashahidi wa mgogoro uliopo wilayani Mbozi, kuhusu upigwaji marufuku ununuzi wa Kahawa mbichi (Red Cherry), hivyo hiyo haiwezi kuwa sababu ya Kimolo kumchefua yeye gazetini.
 
Amesema kwa kuwa hilo halikuelezwa na Kimolo, bali mwandishi huyo wa Tanzania Daima, ameamua kuliweka na kumchafua basi atafuata taratibu kwa kukutana na Kamati ya Maadili ya Chama Cha Waandishi wa Habari Mbeya, ili kuliweka sawa.
 
Ameongeza iwapo hatatendewa haki basi atafuata utaratibu mwingine kwa kulifikisha hilo mbele ya Baraza la Habari Tanzania , kwa hatua zaidi ili aweze kutendewa haki kwa kuchafuliwa mbele ya umma.

Kimolo ametangaza uamuzi huo  (Mei 4) katika kikao chake na waandishi wa habari kilichofanyika katika hoteli ya Beaco iliyopo Forest mpya jijini Mbeya.

No comments:

Post a Comment