Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, May 25, 2012

WANAWAKE TAMBUENI WAJIBU WENU-MBUNGE


MBUNGE wa Nkasi Kusini Desderius Mipata amewataka akina mama kuzitambua haki zao ili kuleta ustawi katika jamii na kuondokana na hali ya kuonekana kama watumwa mbele za waume zao.

Mipata alitoa changamoto hiyo alipokuwa akichangia moja ya mada katika mdahalo wa kujadili masuala ya Jinsia,Haki za wanawake na watoto uliofanyika katika kata ya Kipande ukiwa umeandaliwa mtandao wa asasi zisizo za kiserikali wilayani Nkasi(NKANGONET) na kudhaminiwa na shirika la The Foundation for Civil Society.

Mipata alisema ni kutokana na wanawake wengi nchini kutozitambua haki zao wameendeleo kuonekana kama vibarua hasa kwa waume zao mara tu wanapoolewa dhana aliyosema imepitwa na wakati.

Alisema ni wakati sasa kwa wanawaake kusimamia haki zao ili wawawezeshe pia waume zao kuzitambua na kuzithamini haki hizo na hatimaye jamii itaishi kwa misingi ya kutambua umuhimu wa kila jinsi kwa nyingine.

Mbunge huyo alilalamikia pia unyanyasaji unaofanywa dhidi ya wazee akisema licha ya kufanya kazi kubwa ya kuzitumikia familia na kulijenga taifa lao mpaka kufikia umri wao bado hawathaminiwi kabisa.

Alisema wazee wameendelea kunyimwa haki zao za msingi ikiwemo ya kuishi pasipo kubughudhiwa badala yake kutokana na ugumu wa maisha unaowakabili wanaitwa wachawi eti tu kwakuwa wanamacho mekundu.

Alisema pamoja na changamoto zote hizo bado pia wazee wanapewa mzigo wa kulea wajuu waliozalishwa hovyo na watoto wao na kuwatelekeaza wakati ilipaswa uwe wakati wao kulelewa na watoto hao.

Naye mmoja wa wadau waliohudhuria mdahalo huo mzee John Kauzeni alilalamikia serikali kwa kutotimiza ahadi ya kutoa matibabu bure kwa wazee akisema iliishia kutoa vyeti vya uzee pekee lakini kila wanapokwenda kupata matibabu wamekuwa wakiambiwa hakuna dawa.

“Wengi tuliisifia sana serikali yetu baada ya kutoa vyeti vya kututambua wazee na kuagiza yawepo madirisha maalumu kwaajili yetu.Lakini utekelezaji wa sera hii hauonekani.Kila ukienda unaambiwa hakuna dawa na unatakiwa ukanunue katikaa maduka ya watu binafsi” alisema.

Kwa upande wa elimu kwa toto,ilijadiliwa upo utofauti mkubwa kati ya yule aliyeishia kidato cha nne na hakufaulu ikilinganishwa na aliyeishia darasa la saba.

No comments:

Post a Comment