MKIMBIZA mwenge mkuu kitaifa Olnest Mwanosa
ameikataa taarifa ya ujenzi wa ofisi ya afisa tarafa ya Ilongo wilayani Mbarali
kutokana na ujenzi huo kutoendana na kiasi cha fedha kilichotumika.
Mwanosa aliikataa taarifa hiyo mara baada ya kuweka
jiwe la msingi katika jingo hilo ambalo ujenzi wake ulianza Juni 2011 na mpaka
sasa zaidi ya shilingi milioni 28 zimetumika.
Awali akisoma taarifa ya ujenzi wa jengo hilo kwa
niaba ya afisa tarafa,afisa mtendaji wa kata ya Chimala alisema hadi kukamilika
kwa ujenzi huo zaidi ya shilingi milioni 31 zitatumika.
Lakini Mwanosa alipinga matumizi hayo ya fedha
akisema kiasi kilichotumika ni kikubwa ikilinganishwa na kazi inayoonekana
kufanyika hivyo ipo haja ya wahusika wa ujenzi huo kutoa majibu yatakayoondoa
hoja ya matumizi mabaya ya fedha zilizotengwa.
Alizitaja kasoro zinazoonekana katika jingo hilo pamoja
na udogo wake ikilinganishwa na fedha zilizotengwa kuwa ni kuta kuanza kupasuka
nyufa hata kabla ya ofisi kuanza kutumika,fremu za madirisha na milango
kutokuwa na vigezo vinavyostahili kwa jingo kama hilo.
“Hata kwa hesabu ya kawaida mtu binafsi ukampa
milioni 30 hawezi kujenga kajengo kama haka,lazima ataibuka na jingo kubwa,la
kisasa na linalopendeza sasa mpaka leo zimetumika zaidi ya milioni 28 kwa jingo
hili dogo namna hii.Hapa napata sababu ya kuwa na shaka kuwa huenda kuna mbinu
chafu ya mtu kupitujenzi huu nay eye akawa anajenga kwake”
“Tumepita pale Vwawa wilayani Mbozi kule tulizindu jengo
pia la afisa tarafa ambalo wametumia fedha kidogo sana mpaka kukamilisha pamoja
na samani za ndani.Linapendeza na kweli ukiona unaridhika kuwa kazi imefanyika
sasa iweje ninyi mtumie fedha zote hizo kwa jingo kama hili nab ado halijakamilika
jamani” alihoji.
Aliuagiza uongozi wa halmashauri ya wilaya hiyo
kujipanga upya kwa kuhakikisha mkandarasi aliyehusika na ujenzi wa jengo hilo
anarudia kazi yake vinginevyo hatua zaidi za ufuatiliaji zitachukuliwa.
Aliwaasa viongozi kuwa makini katika ufuatiliaji wa
maendeleo ya miradi mbalimbali kwenye maeneo yao badala ya kubaki ofisini na
kusabaisha serikali iendelee kupakwa matope kutokana na miradi kutoendana na
fedha zinazotumika.
No comments:
Post a Comment