Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Monday, September 29, 2014

ASKOFU MWELA ASHEREHEKEA KUTIMIZA MIAKA 60 YA KUZALIWA




 Askofu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Nyanda za juu kusini,John Mwela akiwa katika ibada ya shukrani kwa kutimiza umri wa miaka 60 huku mkewe Mama Elizabeth Mwela akiwa akisherehekea kutimiza miaka 50.Ibada hii ilifanyika jumapili hii katika kanisa kuu la Anglikana lililopo Uhindini jijini Mbeya.
Wanakwaya wa kanisa kuu wakimpa mkono Askofu Mwela kama ishara ya kumpongeza na kumtakia maisha marefu zaidi
 Ushukuriwe Ee Mwenyezi Mungu kwa kumjalia Askofu huyu kutimiza umri wa miaka 60 huku akionekana kuwa na nguvu zaa kuendelea kukutumikia
Kwaya ya Chisomo kutoka nchini Malawi wakimuimbia bwana Mungu katika ibada hiyo ya shukrani.Kwaya hii iliyoimba nyimbo zake kwa lugha ya nchini Malawi ilikuwa kivutio kikubwa kwenye ibada hii.


Mhubiri na muandaaji wa vipindi vya dini katika redio mbalimbali mkoni Mbeya Victoria Kalengo akihubiri kwenye ibada hiyo ambapo aliwasihi vijana kumkumbuka Mungu siku za ujana wao.


Askofu Mwela akikabidhiwa fimbo kwaajili ya kumsaidia kutembelea iwapo kuna siku afya yake itatetereka kutokana na kuwa na umri mkubwa

Baada ya Ibada sasa sherehe ikahamia nyumbani kwa Askofu huko maeneo ya RRM jijini Mbeya.
Kisha keki maalumu iliyoandikwa kumpa Bwana Shukri ikawekwa mezani.
Hapa Askofu Mwela na Mkewe Mama Elizabeth Mwela wakikata keki tayari kwa kulishana na kuwalisha watu wengine
Askofu Mwela akionesha upendo kwa mkewe kwa kumlisha kipande cha keki.
Mke wa Askofu akionesha upendo wa dhati kwa kumlisha keki Mumewe,Jambo la kumshukuru Mungu pia ni kuwa ndoa ya wawili hawa imetimiza umri wa miaka 25,hivyo.Shukrani hii ilibeba jubilei ya mambo mengi.





















Kwa niaba ya jopo zima la Lyamba Lya Mfipa,mhariri mkuu wa Blogu hii Bw.Joachim Nyambo anaitakia maisha yenye baraka tele familia ya Askofu Mwela.Mungu na Awabariki nyote!

No comments:

Post a Comment