Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Monday, September 15, 2014

WAHAMIAJI HARAMU WAKAMATWA MBEYA



POLISI mkoani Mbeya inawashikilia wahamiaji haramu sita raia wa nchi za Ethiopia,Kongo DRC na Burundi kwa tuhuma za kuingia nchini bila kibali.

Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoani Mbeya Ahmed Msangi wanaoshikiliwa ni Zainabu Asseta(29) na Kadeh Wahalu(27) wote raia wa Ethiopia.

Wengine ni mtoto Jackline Uhasu(7) na wengine waliofahamika kwa jina moja moja ambao ni Devine(25) na Beatha(30) raia wa Burundi na raia wa kongo aliyefahamika kwa jina moja pia la Oliver(25).

Kamanda Msangi amesema wahamiaji haramu hao wamekamatwa Septemba 14,majira ya saa 2:50 usiku katika kijiji cha Mkola tarafa ya Kiwanja wilayani Chunya.

Amesema wahamiaji hao walikamatwa wakiwa wanasafirishwa kwenye basi lenye namba za usajiri T 791 ACJ aina ya Scania mali ya kampuni ya Super Service lakini hakuweza kubainisha ni wapi wahamiaji hao walikuwa wakitokea na wapi walikuwa wakielekea.

No comments:

Post a Comment