Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, September 5, 2014

KIKAO CHA KUPITIA NA KUJADILI TAARIFA YA CAG WILAYANI CHUNYA

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro akisisitiza jambo wakati wa kikao.












WATAALAMU katika halmashauri za wilaya mkoani Mbeya wameagizwa kutumia utaalamu wao kuzuia hoja za mkaguzi na mdhibiti wa fedha za serikali(CAG) badala ya kutumia utalamu huo kujibu hoja.

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro ametoa agizo hilo kwa nyakati tofauti alipokuwa katika vikao vya kupitia na kujadili taarifa ya CAG kwa halmashauri za wilaya za Chunya na Mbeya kwa mwaka wa fedha 2012/2013.

Kandoro amesema ni kwa miaka mingi sasa wataalamu katika halmashauri za mkoani hapa wamekuwa wakionesha umahiri mkubwa katika kujibu hoja zinazoibuliwa na CAG lakini wamekuwa wakishindwa kuonesha umahiri huo kuzuia hoja zisiibuliwe.

Amesema ni wakati sasa kwa wataalamu hao kuziwezesha halmashauri kutokumbwa na hoja kwa kuonesha umahili wanaoutumia kujibu hoja kuzuia hoja kuibuliwa kwa kutekeleza wajibu wao wa msingi.

Kufuatia uzembe huo,kandoro ameyaagiza mabaraza ya madiwani kuhakikisha wanawawajibishwa wale wote watakaosababisha halmashauri zao kupata hoja kutokana na uzembe wa mtu mmoja.

Amesema serikali haiwezi kuendelea kufumbia macho uzembe unaofanywa na watu wachache na kuzisababishia halmashauri kuendelea kuwa na hoja zisizo za msingi na wakati mwingine kusababisha kupata hati chafu.

Amesema kuwajibishwa kwa watu wanaosababisha kuwepo kwa hoja za namna hiyo kutatoa fundisho kwa wengine kuanza kuwajibika ipasavyo wakitambua kuwa uwepo wao katika halmashauri husina kunapaswa kudhihirishwa kwa kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa taratibu za kazi na si ubabaishaji.

No comments:

Post a Comment