Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Thursday, September 4, 2014

NHC KUSAIDIA JIJI LA MBEYA KUWA NA MUONEKANO MZURI BAADA YA WATAALAMU WA JIJI KUSHINDWA




ILI kuwezesha jiji la Mbeya kuwa katika mpangilio na muonekano mzuri,shirika la nyumba la taifa(NHC) limejitolea kutoa ushirikiano wa kitaalamu kwa halmashauri ya jiji hilo.

Mkurugenzi mkuu wa NHC Nehemea Mchechu alisema jana kuwa jiji la Mbeya halipo katika muonekano mzuri kutokana na ujenzi kufanyika kiholela huku akisema yawezekana halmashauri ya jiji hilo halina wataalamu wanaoweza kusaidia kuondokana na adha hiyo.

Mchechu amesema ni malengo ya NHC kuona miji nchini inakuwa katika muonekano wenye kuvutia na kuendana na hadhi stahili badala ya miji na majiji kuwa katika mpangilio usiofaa.

Kwa upande wake meya wa jiji la Mbeya Athanas Kapunga amekubaliana na ushauri huo na kusisitiza kuwa halmashauri iko tayari kuwashirikisha wataalamu wa NHC ili kuweza kutumia utaalamu wao katika kuliboresha jiji hilo.

Kapunga pia amesema halmashauri ya jiji iko tayari kutoa ardhi kwaajili ya NHC kujenga nyumba zitakazowezesha jiji kuwa na mvuto zaidi ya ilivyo hivi sasa.

No comments:

Post a Comment