JESHI la polisi mkoani Katavi
linawasaka watu wanaodaiwa
kumuua kikatili mkazi wa kijiji cha Kapalala wilayani Mlele ,Rehema
Msole(32) kwa kupigwa
na shoka mawe na nondo
na kisha mwili wake kuchomwa
moto wakimtuhumu kuwa mchawi
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari amesema tukio hilo lilitokea kijijni hapo ,Septemba 13 saa 12 jioni baada la kundi la waombolezaji
kumvamia na kumshambulia kwa kumkata
kwa shoka na kumpiga na nondo mawe fimbo na
kisha waliuchoma mwili wake moto
Kidavashari alidai kuwa siku chache
kabla ya tukio hilo
kulitokea msiba kijijini hapo nyumbani
kwa Christopher Baharia ambaye alifiwa na mtoto wake
aitwaye Elizabeth Baharia
Alifafanua baaada ya kutokea kwa msiba huo kuliibuka
hisia kuwa kuna mtu amemloga
binti huyo wakimshuku Rehema Msole
‘’Inasadikiwa
siku za nyuma wakati
ndugu wa marehemu Elizabeth
walipokuwa wakimuuguza walimuona
Rehema akichugulia dirishani
katika chumba alichokuwa
amelala mgonjwa huyo kabla ya kufikwa na umauti .........Hivyo ndugu hao walihisi kuwa mtu huyo
aliyechungulia dirishani ni mchawi wao
‘’ alidai Kamanda Kidavashari
Aliongeza
kuwa siku moja baada ya
Elizabeth kufariki, Rehema akiwa na familia
yake nyumbani kwa Isaya Kyejo aliona kundi waombolezaji wakitokea
kwenye msibani nyumbani kwa Christopher Baharia ambao walizingira nyumba hiyo huku wakishauriana kilicho kuwa
kimewaleta ndipo walipomvamia
marehemu na kuanza kumpiga kwa nondo shoka
mawe na fombo na kisha mwili wake
kuuchoma moto huku wakidai kuwa marehemu ni mchawi
Kamanda huyo alisema polisi linaendelea na uchunguzi
wa tukio hilo ambapo hadi sasa hakuna watu wala mtu aliyekamatwa
kuhusiana na mauaji hayo.
HABARI HII NI KWA HISANI YA BLOGU YA PEMBEZONI KABISA
No comments:
Post a Comment