Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, September 9, 2014

KYELA WAHUSISHA CHF NA FREMASONS,WENYEWE WAUITA MFUKO WA CHIFU



 Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro akiongeza jambo kwenye kikao hicho akikanya wanaopotosha umma kuwa kujiunga na CHF ni kujiunga na mtandao wa Freemasons
Baadhi ya madiwani wakifuatilia maelekezo ya mkuu wa mkoa


 Wataaalamu wa halmashauri ya wilaya ya Kyela nao hawakuwa nyuma kufuatilia

MKUU wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro amekemea vikali watu wote wanaopotosha umuhimu wa mfuko wa Afya ya Jamii(CHF) wakisema ni njia ya kuwaingia wananchi katika mtandao wa Freemasons.

Kwa wilayani Kyela,kupitia CHF kila mkazi anapaswa kulipia kiasi cha shilingi 5000 ili aweze kupata huduma za afya bure kwa kipindi cha mwaka mzima.

Lakini tafsiri ya bima hiyo kwa baadhi ya wakazi wilayani humo imekuwa ni kuhusisha upatikanaji wa huduma kupitia CHF na mtandao wa Freemasons wakisema haiwezekani watu wakapata tiba kwa kiasi kidogo cha fedha kama shilingi 5000 kwa mwaka mzima.


Akiwa katika kikao cha baraza maalumu la madiwani kilichokuwa kwaajili ya kupitia na kujadili taarifa ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali(CAG) kwa mwaka wa fedha 2012/2013 Kandoro amekemea vikali upotoshaji huo.

Amesema iwapo wapo watu ambao hawahitaji kaya zao kujiunga na mfuko wa CHF basi wanapaswa wakae kimya na kuendelea kugharamia matibabu yao badala ya kuendeleza uvumi na kuipotosha jamii na kuisababishia kuami katika mambo yasiyo na msingi kwao.


Mkuu huyo wa mkoa pia ameagiza uongozi wa wilaya kuhakikisha unatoa maagizo kwa viongozi wa vijiji na kata kuendelea kutoa hamasa kwa jamii kujiunga na mfuko huo ili kupunguza gharama za matibabu.

Aidha ametaka pia kuchukuliwa kwa hatua za kisheria kwa mtu yeyote atakaeendeleza maneno ya upotoshaji akihusisha huduma zitolewazo na CHF na mtandao wa Freemasons kwakuwa mtu huyo atakuwa haitakii mema jamii inayomzunguka.

No comments:

Post a Comment