Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, September 16, 2014

WAELIMISHAJI WA MRADI WA GBV NA VAC WATISHIWA MAISHA

Afisa mradi wa GBV na VAC kupitia kanisa la Anglikana akiwasilisha taarifa za utendaji kazi wa mradi huo unaoendeshwa katika kata za Ilembo na Masoko wilayani Mbeya kwa hisani ya watu wa marekani.




Baadhi ya wajumbe wa kamati za Maendeleo za kata za Ilembo na Masoko,wakifuatilia kwa makifuatilia kwa makini taarifa ya utekelezaji wa mradi wa GBV na VAC ilipokuwa ikiwasilishwa Afisa wa mradi huo kwenye kikao cha tathmini ya mradi.
Mmmoja wa waelimishaji wa mradi wa GBV na VAC getrude Elisha akibainisha namna waelimishaji wa mradi huo wanavyotishiwa maisha na watuhumiwa wa vitendo vya ukatili katika vijiji wanavyofanyia kazi ndani ya kata za Ilembo na Masoko wilayani Mbeya.
Muelimishaji Eslom Nsyesye akibainisha changamoto wanazokumbana wakati wa utekelezaji wa majukumu yao ndani ya kata hizo mbili.

HABARI KAMILI.....

WAELIMISHAJI wa masuala ya kupinga ukatili wa kijinsia(GBV) na ukatili dhidi ya watoto(VAC) katika kata za Masoko na Ilembo wilayani Mbeya wamedai kutishiwa maisha yao na watuhumiwa wa matukio ya ukatili.

Katika kikao kikao kilichofanyika jana kijijini Masoko wilayani hapa,waelimishaji hao kupitia mradi wa GBV unaoendeshwa na kanisa la Anglikana kwa hisani ya watu wa Marekani walisema wana wakati mgumu hivi sasa kwani kutoa kwao elimu kumegeuka shubiri kwao.

Mmoja wa waelimishaji hao Getrude Elisha alisema wamekuwa wakipokea vitisho vingi kutoka kwa watuhumiwa wa vitendo vya ukatili wakiwaonya kutoendelea na tabia ya kuwapa ufahami juu ya hatua gani wachukue watu waliotendewa ukatili.

Getrude alisema hivi sasa waelimishaji hao wanashindwa kutembea wakiwa peke yao hususani nyakati za usiku kwakuwa wanahofu wanaweza kuvamiwa na kujeruhiwa kama si kuuawa na watu wanaowatishia kila kukicha.

“Msaada wetu umegeuka tatizo kubwa kwetu.Tunatishiwa maisha na watuhumiwa wa vitendo vya ukatili.Kwa sasa tunaogopa kutembea.Giza likianza inabidi tuwe tumejifungia majumbani mwetu” alisema Getrude.

Muelimishaji mwingine Eslom Msyesye alisema hofu zaidi kwa waelimishaji inatokana na viongozi waliopewa majukumu ya kulinda amani wakiwemo maafisa watendaji kutowajibika kwa taarifa za matukio ya ukatili wanazopelekewa.

Msyesye alisema waelimishaji wamekuwa wakitekeleza wajibu wao wa kuwapa uelewa watu wanaofanyiwa ukatili lakini bara waathirika wanapochukua hatua ya kutoa taarifa kwa maafisa watendaji taarifa hizo zimekuwa zikiishia katika ofisi za viongozi hao kwa watendaji husika kupewa rushwa na watuhumiwa.

Alisema matokeo ya upokeaji huo wa rushwa imekuwa ni watuhumiwa kuendelea kurandaranda mitaani huku wakijitapa kuwa hakuna hatua zozote zinazoweza kuchukuliwa na kuwanyooshea vidole waliotoa elimu kwa muathirika kuchukua hatua.

Kwa upande wake afisa mradi wa GBV Patrick Kosima alikiri kuwepo na taarifa za waelimishaji kutishiwa maisha na watuhumiwa wa vitendo vya ukatili na kuahidi kupeleka suala hilo katika uongozi wa juu wa wilaya ili kulinda usalama wao

Kosima pia aliwatupia lawama maafisa watendaji wa vijiji na kata akisema wanachangia kuendelea kushamiri kwa vitendo vya ukatili katika jamii wanazoziongoza kwakuwa hawachukui hatua stahili kwa watuhumiwa.

No comments:

Post a Comment