Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, March 20, 2012

AJALI YA BASI LA PRINCE MURO KATIKA PICHA

MTU mmoja amefariki dunia papohapo na wengine 14 kujeruhiwa baada ya basi ya kampuni ya Prince Muro waliokuwa wakisafiria kuacha njia na kupinduka katika barabara ya Tunduma –Mbeya.

Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya Advocate Nyombi amethibitisha kutokea kwa ajari hiyo machi 19 mwaka huu,majira ya 2;30katika eneo la Senjele wilayani Mbozi mkoani Mbeya.
 
Kamanda Nyombi alisema ajari hiyo imehusisha gari yenye namba za usajiri T482 BQV aina ya Tyng mali ya kampuni ya Prince muro ambayo ilikuwa ikiendeshwa na dereva ambaye hakufahamika jina.

Alimtaja marehemu kuwa ni Deusdedit Joseph na kati ya  waliojeruhiwa wapo wanawake 4 na wanaume 10 ambapo wote wamelazwa katika hospitali teule ya  Ifisi iliyopo katika halmashauli ya wilaya ya Mbeya kwa matibabu.

Amesema kuwa uchunguzi zaidi juu ya chanzo cha ajali pamoja na juhudi za kumsaka dereva zinaendelea.

Baadhi ya mabaki ya vitu baada ya ajali hiyo jana usiku

Hili Ndilo Gari la mizigo ambalo basi la Prince Muro lilitaka kulipita, na  baadae kushindwa na kupinduka baada ya kukutana na Gari lengine mbele yake


Shimo hili limechimbika wakati wa ajali hiyo ilipo tokea jana usiku

Hapa ndipo Basi la Prince Muro lilipo taka kuingia na kulikwepa gari hili na kupindukia upande wa pili 

Muonekano wa gari hili la mizigo ambalo limeharibikia bara barani 

Mmoja wa majeruhi ambae alikuwa anatokea Dar es salaam kwenda kuwasalimu ndugu zake Ileje aliye fahamika kwa jina moja tuu la Andendekisye akiwa katika Hospital ya Ifisi Mbeya Muda huu

Baadhi ya Majeruhi walio nusurika katika ajali hiyo wakiwa katika Hospitali ya Ifisi kuelekea katika matibabu na kutazamwa kama wamepata matatizo yoyote.

Hawa ni majeruhi kati ya wale 14

Mganga mkuu wa Hospitali ya Ifisi Dkt. Mbilinyi akiongea na moja ya majeruhi mapema leo.

Majeruhi ambao wamenusurika katika ajali hiyo mbaya wamesema kwamba dereva huyo alikuwa mwendo kasi tangia walipo fika mikumi, Wameendelea kudai kwamba walimpa onyo mala kadhaa lakini hakuweza kuwasikiliza na akaongeza mwendo kasi zaidi mpaka walipo pata ajali hiyo maeneo ya Senjele kuelekea Tunduma.
Mtu mmoja amefariki na wengine 14 wakmejeruhiwa wakiwemo wanawake wanne na wanaume 10

PICHA KWA HISANI YA MTANDAO WA MBEYA YETU

No comments:

Post a Comment