Mtoto aliyefahamika kwa jina la Joseph Yusuph(16) mkazi wa Jacaranda jijini hapa amefikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi Mbeya kwa kosa kumwingilia kinyume na maumbile mtoto mwenzie wa kiume.
Akisomewa shitka hilo na wakili wa serikali Rhoda Ngole mbele ya hakimu mkazi Zabibu Mpangule alidai kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo mach 5 mwaka huu katika maeneo ya Jacaranda.
Mshitakiwa alikana shitaka na kupelekwa katika gereza la watoto baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana, na kesi hiyo itatajwa tena Aprili 5mwaka huu.
No comments:
Post a Comment