Kamati tendaji ya chama cha soka mkoani Mbeya MREFA imepitia taarifa ya kamati ya mashindano na kufikia maamuzi ya kuziwajibisha timu nne kwa adhabu tofauti ikiwemo tatu kati ya hizo kufungiwa kutoshhiriki michuano yoyote katika kipindi cha miaka mitatu mfululizo.
Timu zilizofungiwa ambazo pia zitapaswa kuliopa faini ya shilingi 300,000 kila moja kuwa ni Ubaruku FC ya wilayani Mbarali,Sharp Heroes ya Mbeya vijijini na Red Scopion ya wilayani Kyela huku timu ya Juhudi FC ya Mbeya vijijini akisema itawajibishwa kwa kupewa barua ya onyo.
Timu hizo kwa nyakato tofauti wakati ligi ikiendelea kwenye makundi zilionyesha utovu wa nidhamu kwa kufanya makosa mbalimbali ikiwemo kujitoa wakati ligi ikiendelea.
No comments:
Post a Comment