Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, March 27, 2012

SAFARI ZA NDEGE ZAZINDULIWA SUMBAWANGA.

Mkuu wa mkoa wa Rukwa, Mhandisi Stella Manyanya, akifungua mkutano wa mwaka wa wakurugenzi wa utawala na rasilimali watu na makatibu tawala wasaidizi uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa mkoa huo (RDC) jana mjini Sumbawanga.
Mkuu wa mkoa wa Rukwa, Mhandisi Stella Manyanya akifuatilia moja ya mada katikamkutano wa mwaka wa wakurugenzi wa utawala na rasilimali watu na makatibu tawala wasaidizi uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa mkoa huo (RDC) leo mjini Sumbawanga.
Mkuu wa mkoa wa Rukwa, Mhandisi Stella Manyanya, akizungumza na wananchi wa mji wa Sumbawanga  waliojitokeza katika uzinduzi wa safari za anga jana, pembeni yake ni walimu wawili waliofaulisha vizuri aliyesimama katika ni Morison Kibona wa shule ya Msingi Jangwani na pembeni yake ni Pius Nzwalil wa Sekondari ya Kantalamba. pia walimu hapo walipata ofa ya kusafiri na ndege hiyo kutoka Sumbawanga hadi Mkoani Mbeya.
Mkuu wa mkoa wa Rukwa, Mhandisi Stella Manyanya akiimba nyimbo ya kabila la kifipa sambamba na wanakikundi cha Katandala B cha mjini Sumbawanga jana muda mfupi baada ya kuzindua safari za anga kutoka Dar es salaam hadi Sumbawanga zinazofanywa na ndege ya Auric Air.
Mkuu wa mkoa wa Rukwa, Mhandisi Stella Manyanya akisalimiana wa viongozi mbalimbali wa Serikali muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa mjini Sumbawanga wakati wa uzinduzi wa safari za anga jana.
Katibu tawala wa mkoa wa Rukwa, Salum Chima akijiandaa kushuka katika ndege hiyo jana wakati wa uzinduzi wa safari za anga kutoka Dar es salaam kuelekea Sumbawanga.
Ndege ya Auric Air inayofanya safari kati ya Dar es salaam na Sumbawanga ikiwa imetua katika kiwanja cha ndege cha mjini Sumbawanga muda mfupi kabla uzinduzi rasmi wa safari hizo jana KWA HISANI YA pembezonikabisa.blogspot.com. 

No comments:

Post a Comment