JE 2012 NI MWAKA WA CCM NA VITIMBI?
Siku chache baada ya kamanda wa vijana wa CCM mkoani Mbeya Stephen Mwakajumilo kumwaga sumu ya maneno katika jimbo la Mwakyembe Iringa nako CCM ina Mambo.
Habari zisizo rasmi tunaambiwa wakati kesho chama cha mapinduzi (CCM) mkoa wa Iringa kinakusudia kufanya mkutano wake wa Halmashauri kuu ya mkoa ,wajumbe wa mkutano huo wameonyesha kutofautiana na katibu wa CCM mkoa Bi.Mary Tesha na kupanga kutumia mkutano huo kumweka kitimoto ama kumkataa .
Habari kutoka ndani ya chama hicho mkoani hapo zinadokeza kuwa moja kati ya vikwazo vya CCM kuendelea kukataliwa na wakazi wa Iringa ni kutokana na katibu huyo kufanya kazi kivyake vyake na kutowajali watendaji wengine.
Yasemekana kuwa hata wafanyabiashara na wadau mbali mbali waliokuwa wakichangia chama kwa sasa toka afike katibu huyo wameanza kurudi nyuma na kuwa zipo dalili za CCM mkoa wa Iringa kushindwa vibaya katika chaguzi kutokana na katibu huyo kujijali yeye zaidi kuliko chama na kuomba CCM Taifa kujaribu kufuatilia utendaji kazi wa katibu huyo wa mkoa ambaye wamemfananisha na mfanyabiashara
No comments:
Post a Comment