Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Saturday, February 25, 2012

MARY MWANJELWA AKIRI KASI YA CHADEMA INAZIDI YA CCM

 MBUNGE wa viti maalumu mkoa wa Mbeya dk.Mary Mwanjelwa amekitaja chama cha demokrasia na maendeleo Chadema kuwa chama tishio kwa chama chake cha Mapinduzi CCM.
                        
Mbunge Mwanjelwa amesema Chadema ni chama kinachokuja kwa kasi hali inayotoa changamoto kwa wana CCM kujipanga ili kuendana na kasi za chama hicho iwapo inataka kuendelea kushika dola baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Aliyasema hayo katika nyakati na maeneo tofauti alipozungumza na wanajumuiya ya wanawake wanachama wa ccm UWT katika wilaya za Kyela na Rungwe zilizopo mkoani Mbeya.

“Ukweli ni kuwa pasipo kubadilika tutakuwa na wakati mgumu mno.Maana sasa tupo katika mfumo wa vyama vingi na chama kama Chadema mbio zake ni za kasi zinazitutaka tujipange kwelikweli kukilinda chama chetu ”
                    
Mwanjelwa pia alisisitiza kuwa makundi ndani ya CCM kwa kiasi kikubwa yamekiyumbisha chama na pasipo kuondokana nayo hali inaweza ikawa mbaya zaidi.

Aliwasihi wanachama wa chama hicho kuondokana na dhana ya makundi akisema wanachopaswa kukizungumza hivi sasa ni chama ili waweze kuwa na kauli moja itakayokirejeshea heshi yake na si kuendeleza malumbano yasiyo na tija.

Alisema wapo watu wanaoendelea kuyajenga makundi hayo badala ya kuketi na kujadili mikakati ya msingi lakini lengo la watu hao linaonekana ni kujijengea umaarufu wa kisiasa pasipo kujua mzizi wa kujijenga huko utatokana na uimara wa chama chao.

No comments:

Post a Comment