Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Wednesday, February 22, 2012

DK.BILAL KUANZA ZIARA MKOANI MBEYA


MAKAMU wa Rais Dk.Mohamed Gharib Bilal anatarajiwa kuanza ziara ya siku tatu Mkoani Mbeya kesho kutwa (Feb 24).

Kwa mujibu wa mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro akiwa mkoani hapaatak Dk.Bilal atakagua miradi 10 ya maendeleo ikiwemo ile itakayofunguliwa na kuwekwa mawe ya msingi.

Kandoro alisema makamu huyo wa rais atawasili mkoani hapa majira ya saa 4:00 asubuhi na kulakiwa na mwenyeji wake katika uwanja wa ndege wa Jijini Mbeya.

Amesema baada ya ya kupokea taarifa ya mkoa katika Ikulu ndogo ataelekea wilayani Mbozi atakakozindua miradi miwili na kuzungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara utakaofanyika katika kijiji cha Mlowo wilayani hapo.

Aliitaja miradi hiyo kuwa ni soko jipya la kisasa lililojengwa katika mji mdogo wa Tunduma na kuzindua matumizi ya teknolojia ya maabara rafiki katika shule ya Sekondari Vwawa.

“Siku ya pili ya ziara hiyo, Makamu wa Rais atakuwa kwenye wilaya za Mbeya na Mbarali ambako atatembelea miradi minne ya maendeleo katika wilaya hizo”.

“Miradi hiyo ni kuweka jiwe la msingi katika jengo jipya la kisasa la Chama cha kuweka na Kukopa (Saccos) cha Uwamu lililopo Uyole katika Jiji la Mbeya na kuweka jiwe la Msingi katika Hosteli ya Halmashauri ya Jiji la Mbeya”

“Miradi mingine itakayofikiwa na Makamu wa Rais wilayani Mbarali kuwa ni kukagua ujenzi wa soko la mpunga lililopo Igurusi na kukagua ujenzi wa bwawa la umwagiliaji la Rwanyo”.

Kwa mujibu wa Kandoro, Dk. Bilal atahitimisha ziara yake katika halmashauri ya wilaya ya Rungwe ambako atafungua ofsisi ya umoja wa wakulima wadogo wa chai (RSTGA) Bulyaga, kufungua mradi wa umwagiliaji wa Kisegese na kutembelea shamba darasa la Kasyabone.

Mkuu huyo wa mkoa alisema Dk.Bilal ataondoka mkoani Mbeya Februari 28 kuelekea mkoani Iringa kuendelea na ziara yake mkoani humo.

 Mwisho.

No comments:

Post a Comment