Mkazi wa Kijiji cha Saanane Wilayani Mbozi mkoani hapa,Nicodemu Saanane(50) mkulima ameuawa kwa kukatwa kwa na kitu chenye ncha kali katika sehemu za tumboni,na watu wasiofahamika.
Nyombi amesema kuwa tukio hilo lilitokea febuari 4 mwaka huu majira 4.30 katika kijiji cha Kisanu Wilayani Mbozi mkoani Mbeya.
Amesema kuwa marehemu alitoweka nyumbani kwake tangu febuari 3 mwaka huu majira ya saa 5 asubuhi katika mazingira ya kutatanisha na kuelekea kusikojilikana .
Amesema kuwa chanzo cha mauji hayo ni imani za kishirikina kwani marehemu alikuwa anatuhumiwa na wanakijiji wenzake kuwa mchawi kijijini hapo,na kwamba msako mkali unaendelea kuwabaini watuhumiwa waliuohusika.
No comments:
Post a Comment