Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Sunday, February 19, 2012

UNYAMA ALIOFANYIWA MWANAFUNZI WA TEKU NA ASKARI

Mwanafunzi wa mwaka wa kwanza katika chuo kikuu cha TEKU kilichopo jijini mbeya Daniel  Godluck Mwakyusa (31) aliuawa na Askari wa Jeshi la Polisi PC Maduhu tarehe 14/02/2012 katika sikukuu  ya wapendanao {valentine day].
Indaiwa Marehemu akiwa na wenzake wanne walikuwa katika starehe ya kawaida kama ilivyokuwa kwa wengine walioipa umuhimu siku hiyo.Wakiendelea na starehe yao pale Univesal Pub Uyole polisi waliokuwa doria walikuta vijana hao wakipata vinywaji ndipo waliwatuhumu kuwa ni majambazi ambapo PC Maduhu alimpiga marehemu risasi mbili kwa kutumia bunduki aina ya [SMG].
Inaelezwa kuwapia marehemu aliporwa fedha taslimu kiasi cha shilingi laki tatu pamoja na simu ya mkononiambayo haikufahamika mara moja aina na thamani yake
Kwa mujibu wa baba mzazi wa marehemu huyo  Bwana Pastory Mwakyusa amesema kuwa anasikitishwa sana na kitendo hicho  kilichotokea kwani mwanawe hakuwa na tabia ya wizi au ujambazi  hivyo ameliomba Jeshi la Polisi kueleza sababu ya kumuua mtoto wake.
Jeshi la Polisi lilitoa usafiri wa gari lenye nambari za usajili T 138 AFK aina ya Coster kwa ajili ya kusafirisha Mwili wa marehemu kwenda katika wilaya ya Kyela kwa ajili ya mazishi baada ya uchunguzi wa  daktari kuthibitisha kuwa marehemu ameuwawa kwa risasi.
 
Swali ni je tangu lini jambazi,ama mwizi akagharamiwa na jeshi la polisi namna hiyo?

No comments:

Post a Comment