Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Thursday, February 16, 2012

WAHAMIAJI HARAMU WAKAMATWA RUKWA

                       Kamishna Mkuu wa Uhamiaji Tanzania, Mgnus Ulungi.
 MAOFISA wa Uhamiaji mkoani Rukwa wamewakamata wahamiaji haramu wawili akiwemo aliyekuwa mkimbizi kutoka nchi jirani ya Burundi ambaye aliyerejea nchini na kuishi kwenye kambi ya wakimbizi ya Katumba wilayani Mpanda bila kibali.
Kamanda wa Uhamiaji wa Mkoa wa Rukwa, Wiulson Bambaganya amemtaja mhamiaji huyo haramu kuwa Desiree Sindaigaya (38), ambaye amekamatwa jana akiwa anaishi katika kambi ya wakimbizi ya Katumba baada ya kuingia nchini kinyume cha sheria.

Kwa mujibu wa Kamanda Bambaganya mhamiaji huyo haramu amerejeshwa leo nchini Burundi kupitia kijiji cha Manyovu mkoani Kigoma .
Kamanda huyo wa Uhamiaji amemtaja muhamiaji haramu mwingine kuwa Mohamed Sheikh Mohamed (44) raia wa Kenya mwenye asili ya nchi ya Somalia anadaiwa kuingia nchini na kuishi bila ya vibali vya kusafiria .

Inadaiwa Mohamed amekamatwa jana mchana katika eneo la Lwiche mjini Sumbawanga, baada ya kutoroka akiwa amedhaminiwa mjini Mpanda akihofia mkono mrefu wa Serikali kwa kuingia , kuishi na kufanya kazi nchini kinyume cha sheria .


Kwa mujibu wa Kamanda Bambanganya, alipohojiwa mhamiaji haramu huyo amekiri kuingia nchini bila kuwa na kibali cha kusafiria na kwamba aliweza kuishi na kufanya kazi ya upishi kwa zaidi ya miezi mitatu katika hoteli moja mjini Mpanda, hadi hivi karibuni alipokamatwa kufuatia taarifa za siri kutoka kwa raia wema


Kamanda huyo wa Uhamiaji amesema kuwa muhamiahji huyo haramu anatarajiwa kufikishwa kesho katika Mahakama ya Hakimu Mkazi iliyopo mijini Sumbawanga .

No comments:

Post a Comment